Sunday, August 30, 2015

NAIROBI:THE LIGHTBEARERS WAREKODI NYIMBO KATIKA STUDIO ZA HOPE CHANNEL AFRICA

Copy the BEST Traders and Make Money (One Click) : http://ow.ly/KNIC
Jumla ya Waimbaji 19 wa The LightBearers wako jijini Nairobi,Kenya kwa ziara maalum ya uimbaji ambapo watashiriki kwenye Tamasha la Uimbaji litalofanyika leo jumapili Agosti 30,mwaka kuanzia saa 8:00 mchana hadi saa 12:00 jioni kwenye ukumbi wa Nairobi Cinema. Jana Agosti 29 jioni walikuwa katika studio za Hope Channel Africa zilizopo yalipo Makao Makuu ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Divisheni ya Afrika Mashariki na Kati (ECD) eneo la Ongata Rongai ambapo wamerekodi nyimbo tano za video ambazo zitarushwa na kituo hicho cha Televisheni kinachorusha matangazo yake kupitia satalaiti kwa kushirikiana na Hope Channel International. 
 --------------------------------
Baada ya Tamasha la leo The LightBearers wataelekea jijini Arusha kisha Mwanza ambako watashiriki kwenye tamasha litakaloambatana na kuitambulisha album yao namba 3 iitwayo MUNGU kimbilio tukio litakalofanyika kwenye ukumbi wa Vijana Mlango Mmoja Septemba 5 mwaka huu saa nane mchana.


 Picha/Habari na Mtangazaji Blog
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA