Tuesday, December 09, 2014

DARUBINI YA IMANI
                                        Pr  Dominic  Mapima.
                    Somo - Mahubiri ya hadhara – Morogoro.
HOTELI YA MUNGU DUNIANI
UTANGULIZI
KATIKA DUNIA YETU TUMEONA NA KUTEMBELEA HOTELI MBALIMBALI,HOTELI HIZO ZIMESHEHENI AINA MBALIMBALI ZA VYAKULA NA VINYWAJI VINAVYOONEKANA NI VYEMA NA KUPENDWA NA WATU. KATIKA SOMO HILI TUTAANGALIA JUU YA HOTELI NYINGINE LAKINI JAMBO LA KUSHANGAZA NI KUWA HII SASA NI HOTELI YA MUNGU DUNIANI.
KWANINI HOTELI YA MUNGU?
WAKATI FULANI HOTELI HIZI ZINAZOONGOZWA NA WATU WA DUNIA ZIMEZAA MATOKEO MABAYA KWA WATEJA, MATOKEO AMBAYO YAMEWAPA MAJUTO MAKUBWA NA KULAUMU NIA YAO NJEMA YA KUTAFUTA HUDUMA KATIKA HOTELI HIZO, HIVYO KWA HALI HII NI MUNGU PEKEE ANAWEZA KUWA DIRA KWA WANADAMU KWA KUWAPA KANUNI BORA NA VIWANGO KATIKA SWALA ZIMA LA ULAJI.
KISA:-
Watu fulani walikuwa wakisafiri kuelekea mikoa ya kusini’ muda wa chakula cha mchana ulipofika gari ilipaki na wakaingia kwenye vibanda vya hoteli ndogondogo vilivyokuwa njiani hapo, wakiwa wameketi tayari kwa kula waliagiza supu, pindi wakiendelea kunywa ndipo mmoja wa wateja hao alisikika akiomba kuongeweza nyama!_ghafla alisikia sauti ikijibu toka jikoni na kusema’ “Samahani kaka kaumbwa kenyewe tulikokachinja leo kalikuwa kadogo!!!!!!!!!_ wale wateja walianza kutapika!!!!!!
Tunapozunguzia Hoteli tunazungumzia jengo lililobuniwa na mwanadamu kwaajili ya kutoa huduma ya vyakula, hivyo tunapozungumzia hoteli ya Mungu duniani maana yake ni jengo la Mungu ambamo pia uhusika na ulaji, maandiko matakatifu ya Biblia yanaweka bayana juu ya jengo hilo la Mungu(hoteli)hapa duniani ambamo humo ni vyakula vyenye ubora tu hupaswa kuingizwa na ni kwa kadri ya maelekezo ya mmiliki wa hoteli hiyo, hebu tuone hoteli hiyo na maelekezo yake ya vyakula vinavyopaswa kuingia humo.
Hoteli ya Mungu ni ipi?
Bilblia inaanza kwa kusema:-
1Wakoritho 3:9
Maana si tu wafanyakazi pamoja na Mungu, ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.
Biblia katika fungu hilo inamtaja mwanadamu kuwa ni shamba la Mungu na pia ni jengo la Mungu, hivyo kimsingi mwili huo wa mwanadamu (jengo) ndiyo hoteli ya Mungu duniani katika farsafa ya kiroho, tamko la Yesu akiwa mbinguni kupitia kinywa cha Yohana inapigia mstari farsafa hiyo ya kiroho.
Ufunuo 3:20
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, nayeye pamoja nami.
Tamko hilo la Yesu linabeba dhana nzima ya kimahusiano ya kila nyanja anayokuwa nayo Mungu na mtu aliyeamua kumpokea kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake, neno alilotumia Yesu hapo ni kuwa “mtu akifungua mlango ataingia kwake naye atakula pamoja naye”.
Neno hilo kula pamoja naye pamoja na kuwa lina tafsiri pana sana na ya nyanja nyingi lakini pia inahusika na ulaji wa kawaida kwa kuwa kiukweli katika mafungu mengine Biblia inataja kanuni za kimsingi za ulaji unaokubaliwa na Mungu ambao mtu akiufuata na kuenenda kwa huo basi bilashaka huko ndiko kula pamoja na Mungu. (yaani kula kwa kufuata mapenzi na Baraka za Mungu).
Hivyo Mungu hula pamoja nasi kwa njia ya kudhinisha na kubariki tulacho.
1Wakoritho 6:17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho naye.
Mtume Paulo anaweka mkazo dhana hiyo ya Mungu kujihusha na kila nyanja ya mwanadamu, kwa kusema kuwa sisis tu roho mmoja na Bwana.
Na ndipo baada ya tamko hilo ndipo tena mtume Paulo anafunuliwa kuandika kile kinachobainisha wazi ukweli wa vile Mungu anavyojihusisha na hata na ulaji wetu, na jinsi tunavyopaswa kusikiliza maelekezo yake katika swala la ulaji ili tumtukuze pia hata katika swala la ulaji kwa kuitendea haki hoteli yake yaani miili yetu.
1Wakoritho 10:31
Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lolote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
JE KULA KWA UTUKUFU WA BWANA NI KWA NAMNA GANI?
Yako mambo makuu mawili yanayoweza kutajwa kuwa ndiyo kula kwa utukufu wa Mungu ambayo ni:-
-       Kufuata maelekezo ya kanuni ya ulaji na aina ya vyakula vilivyoruhusiwa na Mungu mwenyewe kuingia katika miili yetu (hoteli yake).
-       Kwakuwa tu roho mmoja na Bwana tusingepaswa kula kwa namna ambayo itakimbiza uwepo wake au kuharibu utukufu wake maishani mwetu.
Kufuatia maelekezo hayo hasa hayo ya kwanza yahusuyo kula kwa utukufu wa Mungu, bilashaka wali linaloibuka hapo ni kuwa je’ basi! Mungu alitoa maelekezo juu ya vile vinavyopaswa kutumika kama vyakula kwa watu wake?
Kumbuka Mungu alisema”
Zaburi 84:11..sitawanyima kilicho chema hao waendao kwa ukamilifu…..
Hivyo Mungu mwenye aliahidi kuwapa wanadamu vyakula vilivyo bora ambavyo kimsingi ndivyo vinavyompendeza yeye mwenyewe pia.
MUNGU ALIPOANZA KUAINISHA CHAKULA NA VISIVYO VYAKULA.
Kama hatua ya kutimiza ahadi yake ya kumpa kilichochema mwanadamu aendae kwa ukamilifu, Mungu kupitia mzee Nuhu’ alianza kuainisha vilivyo visafi na visivyo visafi.
Jambo la msingi la kuelewa ni kuwa hayo yalifanyika kabla ya kunza taifa la Wayahudi (Israel) kwahiyo yalikuwa ni maelekezo yaliyohusu afya ya mwanadamu yeyote na siyo tabaka Fulani la umma./ hebu tusome:-
Mwanzo 7:1-2
Bwana akamwambia Nuhu, Ingia wewe katika safina; kwamaana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki. (2) Katika wanyama wote waliosafi ujitwalie saba saba, mume na mke; na katika wanyama wasio safi wawili wawili, mume na mke.
Maelezo ya Mungu kwa Nuhu katika andiko hilo yanaweka wazi juu ya vile Mungu mwenyewe aliyeumba namna alivyoweka makusudi yake kwa kila mnyama aliyemuumba, hapo alimaanisha wazi kuwa Nuhu asingepaswa kuwaona wanyama wote katika uwiyano, badala yake kati ya hao wako waliosafi na wasiyo safi na kwa maana nyingine basi hata makusudi ya kimatumizi ya wanyama hao ni tofauti.
Kumbuka killakitu kilichoumbwa kina makusudi yake’
Mfano:
Leo hii wako watu ambao wanakata kope(nywele za juu ya jicho) zao kwa hisia kwamba hazina kazi, lakini kimsingi kope hizo ziliwekwa ili kuzuia maji yenye sumu toka kichwani yanapotelemka kutokea utosini yasiingie moja kwa moja jichoni, badala yake yasukumwe pembeni na kope hizo.
Hivyo kwajumla matumizi ya wanyama hao hayafanani, na ndipo basi tunaposoma Biblia Mungu hapo mbeleni kipindi cha wana wa Israeli aliainisha wanyama hao wazi, yaani wale wanaoliwa na wale wasiyoliwa pamoja na ndege samaki nk.
Lawi 11:1,2,3,4,6,7,8
Bwana akanena na Musa na Haruni ,na kuwaambia, (2) Neneni na wana wa Israeli , mkiwaambia, Wanyama hawa ndiyo wenye uhai mtakaowala, katika hayawani wote waliyo juu ya nchi. (3) Kila mnyama mwenye kwato katika miguu yake, mwenye miguu ya kupasuka kati, mwenye kucheua, katika hayawani, hao ndiyo mtakaowala (4) Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia kwakuwa yu acheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu. (6) Na sungura, kwasababu hucheua, lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.(7) Na nguruwe, kwasababu yeye anazo kwato, nimwenye miguu iliyopasuka kati , lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu, (8) Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni  najisi kwenu.
Hao ndiyo wanyama waliotajwa kwa uwazi kuwa Mungu hakukusudia wawe chakula, kumbuka wakatika ule wa Nuhu tena kabla ya taifa la Wayahudi kuanza Mungu alishaweka bayana juu ya tofauti ya wanyama hao, yaani wako waliyosafi na waisiyo safi.
Lakini pia jambo la kukumbuka ni kuwa wale wasiyo safi waliwekwa ka idadi pungufu ikiwa ni kiashiria kwamba matumizi yao hayakulenga chakula, tendo ambalo Bwana Yesu pia alilidhihidhirisha kama tutakavyoona hapo mbele kidigo.
Kwa habari ya samaki Biblia imeainisha kuwa wale wanaopaswa kuliwa ni wale wenye magamba na mapezi pekee, na ndege pia wametajwa kama unavyoweza kujisomea katika sura hiyo hiyo ya kitabu cha Walami 11:13-20.
JE YESU ALIPOKUJA ALIBADILI KANUNI HIYO YA ULAJI?
Ni jambo linaloshangaza kulisikia toka kwa wachungaji na waalimu mbalimbali wa dini katika madhehebu ya Kikristo, wakidai kuwa ati hiyo ilikuwa ni sheria ya mpito tu na ilihusika na wana wa Israeli pekee na hivyo kwasasa baada ya neema ya Kristo tunaweza kula chochote na hata hivyo vilivyoharamishwa na siyo dhambi.!
Kile kinachoonekana kuwa ndicho kigezo cha tafsiri hiyo yenye utata, ni tendo la Yesu kuatamka kuwa kile kimwingiacho mtu akiwezi kumtia unajisi.
Marko 7:14  kimwingiacho mtu akimtii unajisi…….
Kupitia kisa hicho cha andiko hilo ndipo changamoto ilipoanzia.
Uchunguzi wa kisa hicho.
Ni jambo la msingi kueleweka kuwa kisa hicho kimechukuliwa vibaya na baadhi ya wasomaji hao wa Biblia, na kile kilichowapotosha watu zaidi ni kule kutozingatia kanuni katika usomaji wa Biblia, katika kisa hiki msomaji kwanza akipaswa kuzingatia kanuni kuu mbili za usomaji wa Biblia nazo ni:-
-       Kujua wazo (hoja) kuu jadiliwa katika andiko hilo (discussed matter).
-       Kulinganisha kisa hicho na maandiko mengine ili kupata wazo halisi (comparative study of the Bible ). Mhubiri 7:27… nimeyaona hayo kwa kulinganisha hili na hili ili kutafuta jumla….
Kwa kufuata kanuni hiyo ya kwanza ya kungalia wazo kuu jadiliwa,tunaweza sasa kusoma andiko husika kwa kunzia aya ya kwanza ya kitabu cha Marko ili kuona chimbuko la kisa na nini hasa hoja kuu.
Kujua wazo (hoja) kuu jadiliwa katika andiko hilo (discussed matter).
Marko 7:1-3
Kisha Mafarisayo, na baadhi ya wandishi waliotoka Yerusalemu, walikusanyika mbele yake. (2) Wakaona wengine katika wanafunzi wake wakila vyakula kwa mikono najisi, yaani, isiyo nawiwa. (3) Maana Mafarisayo na Wayahudi wote wasiponawa mikono mpaka kiwiko, hawali, wakishika mapokeo ya wazee wao.
Mpendwa msomaji wangu ni imani yangu kuwa hoja hii sasa aitakuwa tatizo kwako, kumbe kile kichopelekea Bwana Yesu kutoa kauli hilo ilikuwa ni kujibu hija hii mahsusi ambayo ilikuwa na mtazamao wa kufanya mapokeo ya wazee yasiyo neno la Mungu kuwa ndiyo mwongozo wa maisha ya mitume wa Yesu, kama tulivyosoma kuwa kile kilichokuwa chanzo cha hoja hiyo ni matakwa ya Wayahudi na Mafirisayo kuwaona mitume wakinawa hadi kwenye viwiko ili kufata mapokeo hayo ya wazee wao.
Katika tukio hilo ieleweke kuwa hapakuwa na chakula najisi kilichokuwa kikiliwa na mitume, bali Mafarisayo walitaka kuanzisha aina yao ya unajisi inayotokana na kula bila kunawa hadi kwenye kiwiko cha mkono, hivyo kauli ya Yesu kuwa kimwingiacho mtu hakimtii unajisi ililenga kile kinachotokana na kula bila ya kunawa kwa taratibu walizotaka wao na si kuwa Yesu alimaanisha vyakula ambavyo tayari viliitwa najisi.
Kauli ya Yesu mwenyewe alipokuwa akihitimisha tamko lake inafunga mjadala huu:-
Mathayo 15:20
Hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hujanawa mikono hakumtii mtu unajisi.
Hitimisho hilo la Yesu katika kisa hicho ni jibu tosha kuwa hakuwa akitoa tamko la jumla la kuruhusu vyakula najisi badala yake hoja ilikuwa ni kula bila kunawa.
Lakini pamoja na hayo, kama Yesu alimaanisha kuwa ni chochote kikimwingia mtu hakimtii unajisi, basi maana yake ni kuwa hapo Yesu alikuwa akihalalisha vitu vungi ikiwemo Pombe katika aina zake ambazo hutoka kwa njia ya mkojo, huenda sigara, bangi nk ambavyo navyo haviingii moyoni.
-       Kulinganisha kisa hicho na maandiko mengine ili kupata wazo halisi (comparative study of the Bible ). Mhubiri 7:27… nimeyaona hayo kwa kulinganisha hili na hili ili kutafuta jumla….
Kanuni hiyo ya pili iliyokiukwa na wale wanaohalalisha vilivyoharamishwa kwa kutumia mgongo wa tamko hilo la Yesu ingeweza kuwa msaada mkubwa endapo wahusika wangekubali kuitumia katika kutafuta ukweli wa swala hili, katika andiko hilo mhubiri anasema “nimeyaona hayo kwa kulinganisha hili na hili ili kutafuta jumla (Mh 7:27).
Kwa kutumia kanuni ya kulinganisha maandiko utagundua kuwa kamwe tamko la Yesu halikulenga  Kuruhusu vitu alivyovikataza kuwa visiliwe na kuvifanya kustahili, pia ikumbukwe kuwa kuzuiwa kwa vyakula hivyo yaani baadhi ya wanyama ndege na  samaki haikuwa adhabu kwa wanadamu bali ilkuwa ni kwa sababu za kiafya na makusudi yake ya uumbaji wa viumbe hivyo kwamba baadhi yake aliona kuwa visingefaa kuwa chakula.
Zaburi 84:11..sitawanyima kilicho chema hao waendao kwa ukamilifu…..
Isaya 55;14…kwani kutoa fedha kwa kisicho chakula?...
Jinsi Yesu alivyoendelea kuainisha vyakula na visivyo vyakula.
Hili ni jambo linalo nishangaza sana, inaniwia vigumu kuamini kuwa wachungaji na waalimu mbalimbali katika madhehebu za Kikristo hawajawahi kulisoma andiko hili la Luka na kujionea wenyewe tamko hili la Yesu na jinsi alivyoainisha vyakula na visivyo vyakula yeye mwenyewe:-
Mathayo 7:9 -11
Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye mwanawe akimuomba mkate, atampa jiwe? (10)Au akiomba samaki, atampa nyika? (11) Basi ikiwa ninyi ,mlio waovu,mnajua kuwa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wampendao?
Katika andiko hilo kama ulivyoona Bwana Yesu anaainisha kati ya vyakula na vuisivyo vyakula, sehemu ya kwanza aya ya 9’ anaonyesha kuwa mkate ni chakula na jiwe si chakula na hivyo haistahili kumpa motto jiwe. Aya ya 10’ anaonyesha tena kuwa samaki ni chakula lakini nyoka si chakula na haistahili kumpa mototo nyoka aombapo chakula.
Sasa kwa maelezo hayo ya Yesu wale wanaodai kila kitu kimehalalishwa wanatumia ushahidi gani kuthibitisha madai hayo?
KWA UJUA HAKIKUWA CHAKULA YESU ALIANGAMIZA NGURUWE’.
Miongoni mwa mambo ya msingi ya kujifunza kwa Yesu juu ya mpango wake wa vyakula katika hoteli yake ni tukio hilo la kuangamiza nguruwe, ili kuelewa ujumbe wa Yesu katika katika tukio hilo rejea kwa kutafakari matukio mbalimbali ya huruma aliyoyafanya Yesu kwa kuwapa watu chakula kama vile:-
-       Muujiza wa ongezeko la mikate na kulisha watu wengi.
-       Muujiza wa ongezeko la samaki pamoja na kuwawezesha kina Petro kupata samaki baada ya kuhangaika usiku kucha.
-       Muujiza wa kugeuza maji kuwa divai ili kunywesha watu arusini.
Matukio hayo yote yanaonyesha jinsi Yesu alivyokuwa na moyo wa huruma kwa watu pale ambapo inaonekana wametindikiwa na chakula. Lakini katika tukio hili tunaona Yesu anafanya kinyume pale alipoamuru kundi kubwa la nguruwe kuingiwa na mapepo na kufia ziwani.
Luka 8:32-33
Basi, hapo kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani,; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale, akawapa ruhusa. (33) Pepo wakamtoka mtu yule wakawaingia nguruwe, nalo kundi likatelemkia gengeni kwa kasi, wakaingia ziwani, wakafa maji.
Kimsingi huu ulikuwa ni ujumbe wa kimya wa Yesu ambao kimsingi unaungana na kile tulichosoma katika kitabu cha Mwanzo juu ya idadi ya wanyama aliotakiwa kuwaingiza katika safina, kumbuka Mungu alimwambia wale wanyama walio safi aingize saba saba na wasiyo safi wawili wawili, hivyo kwa muktadha wa tukio hilo la Yesu kungamiza nguruwe tunaona mwakozi akifanya kile kile ambacho aliamuru kifanyike wakati wa Nuhu, kumbuka wakati pia idadi ya wanyama wasiyo safi ilipaswa kupungua na hapa sasa Yesu anaamuru kupungua kwa idadi wa wanyama hao ambao si chakula katika mji ule wa Gerasi.
2Wakoritho 6:17-18
kwahiyo,Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.(18) Nitakuwa Baba kwenu nanyi mtakuwa kwanu wanangu wa kiume na wakike

Tafakari upya na fanya matengenezo juu ya ulaji ili ule vile vinavyo mpendeza Bwana.



















****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA