SONDA
YA DIHLU ni kundi linapatikana DAR ES SALAAM – TANZANIA katika
kanisa la WAADVENTISTA
WASABATO UKONGA. Kundi hili
linahubiri injili kwa njia ya Uimbaji wa muziki wa Injili aina ya Acapella yaani
muziki uimbwao bila kutumia vyombo vya Muziki.
Jina SONDA YA DIHLU linatokana na lugha ya KISUKUMA likiwa
na maana ya NYOTA YA ASUBUHI kwa Kiswahili.
Kundi hili lilianza rasmi 16/09/2006
likiwa na jumla ya waimbaji watano ( 5 ).
ISAYA DANIEL ( Lead/ Second Tenor
), ELISHA BARNABA ( First Tenor ), BAEL DISHON ( Baritone ), JIMSON
MLOWE ( Second Tenor ) na EMANUEL
TUNZO ( Bass ), chini y a uongozi wake BAEL DISHON (Mwenyekiti), ISAYA DANIEL
(Katibu).
Na mnamo mwaka 2007 Kundi
lilifanikiwa kurekodi Albamu ya kwanza inayojulikana kwa jina la “HUKUMU”
iliyorekodiwa “ MALAIKA RECORDING STUIDIO” na kurudiwa mwaka 2008 na “MORNING STAR FM RECORDING STUDIO”. Na mwishoni mwa mwaka 2011 kundi
lilifanikiwa kurekodi albamu ya pili inayojulikana kwa jina la “HALLELUYA
TUKIFIKA JUU”. Kwa sasa kundi lina jumla ya waimbaji saba ( 7), ISAYA DANIEL ( Lead/second Tenor ), ELISHA BARNABA ( First Tenor ), MSAFIRI TUNZO ( Baritone ), JIMSON MLOWE ( Second Tenor ), RICHARD YESSAYA ( Bass ), EMMANUEL TUNZO ( Bass ), na JACKSON FANUEL (Lead/Second Tenor), Chini ya
uongozi wake ELISHA BARNABA( Mwenyekiti), JIMSON MLOWE (Katibu), na MSAFIRI
TUNZO (Mhazini). Kundi hili tangu
kuanzishwa kwake limekuwa likihudumu
katika mikutano mbalimbali kama
vile MAHAFALI ZA ASSA NA THISDASO, MIKUTANO YA INJILI YA HADHARA (EFFORTS ),
MIKUTANO YA MAKAMBI, SABATO MAALUM ZA WAGENI na MATAMASHA MBALIMBALI YA NYIMBO
ZA INJILI, NDOA NA HARUSI MBALIMBALI,
PAMOJA NA HUDUMA MBALIMBALI ZA KIROHO NA KIJAMII, ndani ya nchi katika
maeneo ya MOROGORO, MBEYA, ZANZIBAR, MTWARA, PWANI, DAR ES SALAAM, na nje ya
Nchi kama; KAMPALA nchini UGANDA ( WORLD MUSIC-FESTIVAL)Mwaka-2010-na NAIROBI,
NAKURU nchini KENYA Mwaka 2011.
Kuihubiri Injili ya YESU kwa kasi na katika mazingira
yeyote yale, mahali popote duniani,
mpaka YESU anaporudi mara ya pili kutuchukua kwenda mbinguni.
DIRA YAO
Kuwa kundi bora linalofikika na kuwafikia watu kwa
Wepesi na urahisi zaidi popote duniani, pia kuwa na “Recording Studio” Kubwa.






0 comments:
Post a Comment