![]() |
| Kushoto ni bibi Nancy mke wa raisi wa wasabato ulimwenguni na Kulia ni Raisi wa wasabato ulimwenguni ndugu,Ted NC Wilson HABARI NA ANN(ADVENTIST NEWS NETWORK) |
Rais wa waadventista
wasabato Ted NC Wilson atoa rambirambi kwa familia za wale waliouawa katika mashambulizi
ya wapiganaji nchini Kenya Novemba 22. Katika shambulio hilo la watu 28 waliokua
kwenye bus hilo miongoni mwao walikua ni waumini wa
kanisa la kiadventista la wasabato, Rais wa waadventista wasabato Ted NC Wilson alisema
yafuatayo wakati anatoa mchango wake wa
Rambi rambi.
========
Kwa niaba ya ya waumini Wakisabato ulimwenguni mzima, tumesikitishwa
sana na vifo vya kutisha huko nchini Kenya na ukiangalia katika shambulio hilo
kuna wengine ni waumini wa kanisa hili la kisabato Mioyo yetu imejaa majozi makubwa sana hasa kwa familia ambazo wamepoteza wapendwa wao,
wakiwemo watoto, katika mauaji ya kikatili.
Mke wangu, Nancy, na yeye anapenda kutoa
salamu za rambirambi kwa familia za
Kikristo zilizokumbwa na tatizo hilo.Hatuwezi kuelewa nikwaniani mauaji ya kutisha yamechukua nafasi kubwa nchini Kenya .
Hata hivyo, Roho Mtakatifu kama Msaidizi inaweza kuleta faraja kwetu. Mim na
familia yangu nimejitolea kuwaombea familia hizi zilizo kumbwa na hili tatizo
la kuondokewa na wapendwa wao.
=========
Ni baraka kujua kwamba katika siku za usoni, wakati Yesu atakaporudi, Naye atafuta kila aina ya machozi. Wafilipi 4: 7 inasema, ". Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu"
Ni baraka kujua kwamba katika siku za usoni, wakati Yesu atakaporudi, Naye atafuta kila aina ya machozi. Wafilipi 4: 7 inasema, ". Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu"
Pamoja na mauaji katika ulimwengu huu wa sasa, kuna matumaini
ya baadaye wakati Kristo atarudi. Kwa uwezo wa Mungu, hebu kuwa waaminifu kwa Neno
lake na kwake! Nini faraja kujua kwamba kurudi kwa Yesu Kristo ni kumekaribia na
tunaweza kuhesabu tumaini la Kikristo uzima wa milele.
==========
Naomba kutoa salamu hizi za rambi rambi kwa familia zote zilizo kumbwa na
tatizo hili na Mungu awe mfariji mkuu katika tatizo hili. Amen




0 comments:
Post a Comment