Wednesday, December 03, 2014


Wanafunzi  sabini na watatu (73) wameweka rekodi ya wanafunzi wa kisabato kubatizwa katika shule moja mwaka huu katika kisiwa cha vanatu. Idara ya vijana katika kisiwa cha vanatu imeripoti kua  lilifanyika juma la Maombi shuleni lhapo kwa muda wa wiki tatu katika shule hiyo na liliongozwa na mchungaji Charlie Jimmy pia wanafunzi hao waliweza  kuyapenda masomo hayo nakuanza mafunzo ya kujifunza biblia rasmi kwa ajili ya ubatizo
Pia kutokana nawanafunzi  kukubali masomo hayo mwezi oktoba mwaka huu  mchungaji Charlie Jimmy ambaye anafanya kazi katika ofisi ya mkuu Mission ya Vanuatu katika Port Vila, walirudi kisiwa cha Santo kubatiza wanafunzi  ambao walimkiri Yesu kua Bwana na Mkombozi wa Maisha yao.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya Aore Alisema “Amefurahishwa sana kuona kua wanafunzi hao wame mpokea Yesu na kumkiri kua ni Bwana na Mkombozi wa Maisha yao “Pia aliongezea nakusema kua wanafunzi hao wamekua mfno mkubwa katika shule hiyo na si katika  masomo darasani hata katika upande wa kiroho.

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA