MKATABA
wa kujenga tena umoja na kukiunganisha upya Chama Tawala cha Sudan Kusini cha Sudan People’s Liberation Movement (SPLM)
ulitiwa saini usiku wa jana, Jumatano, Januari 21, 2015, katika sherehe ya
kufana iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Ngurdoto, .
Sherehe
hiyo ilishuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho
ndicho kimesimamia mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo. Rais Kikwete pia ndiye
mdhamini mkuu wa Mkataba huo.
Mkataba
huo pia unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinabuni na kutekeleza sera za
kuondokana na ukabila, makundi yenye mitazamo finyu na mwenendo wa kijeshi
katika siasa za Sudan Kusini.
Aidha,
Mkataba huo unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinafanya mageuzi ya
kuanza kujenga utamaduni wa kuvumiliana na ujenzi wa misingi ya demokrasia.
Mkataba
huo pia unataka watu wote ambao walishiriki katika mauaji na umwagaji damu
katika vita vya wenyewe kwa wenyewe wasiruhusiwe kugombea wala kushika nafasi
ya uongozi wa umma ndani ya chama hicho.
Pia
viongozi wote wa Sudan Kusini wanatakiwa, chini ya Mkataba huo, kuwaomba radhi
wananchi wa nchi hiyo ya Sudan Kusini kwa kuruhusu nchi hiyo kuingia katika
machafuko ya umwagaji damu mkubwa.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
– Dar es Salaam.
22 Januari,2015

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akikaribisha viongozi na wajumbe katika mkutano huo

Waziri Mkuu Mstaafu na Makamu Mwenyekiti wa zamani wa CCM Mheshimiwa
John Samwel Malecela ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa mazungumzo yaliyozaa
Mkataba huo akisoma muhtasari wa mazungumzo hayo
Sehemu ya ukumbi wa mkutano huo

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza utiaji wa saini wa Mhe. Salva Kiir Mayardit Rais wa Sudan Kusini ambaye pia ni Mwenyekiti wa SPLM na anayeongoza kundi linalojulikana kama SPLM in Government (SPLM-IG), Mheshimiwa
Dkt. Riek Machar ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa SPLM na pia
aliyekuwa Makamu wa Rais wa Sudan Kusini anayeongoza kundi la SPLM in Opposition (SPLM-IO) na Dkt. Deng Alor Kuol ambaye anaongoza kundi la SPLM Leaders- Former Detainees (SPLM Leaders – FD).

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) na Bw. Deng Alor Kuol wakionesha hati baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa pongezi kwa Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) na Bw. Deng Alor Kuol
baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wakati Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na
kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wakati Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na
kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.

Rais Yoweri Museveni wa Uganda akiongea

Dkt. Riek Machar akiongea

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya akiongea
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Naibu Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa (kulia) na Bw. Bw. Deng Alor Kuol wakifurahia wakati Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (wa pili kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
Rais Salva Kiir Mayardit wa Sudan ya Kusini
Rais Salva Kiir Mayardit wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa
Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono
na kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano
ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.

Rais Kikwete na Bw. Dkt Kuol wakipiga makofi wakati Rais Salva Kiir Mayardit wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny wakipeana mikono kwa furaha baada ya kutia saini mkatana wa makubaliano ya kukiunganisha
upya chama cha SPLM cha Sudani Kusin

Naibu Rais wa Afrika ya Kusini Mhe Cyril Ramaphosa akiongea na kupongeza hatua iliyofikiwa

Rais Kikwete akiongea na viongozi na wajumbe katika mkutano huo

Rais Kikwete akiongea na viongozi na wajumbe katika mkutano huo

Rais Kikwete akiongea na viongozi na wajumbe katika mkutano huo

Rais Kikwete akiongea na viongozi na wajumbe katika mkutano huo

Wajumbe wa kundi la SPLM
in Opposition (SPLM-IO)

Sehemu ya wajumbe wa kundi la SPLM in Opposition (SPLM-IO)
Kila mtu alisimama kumshangilia Rais Kikwete
Wajumbe wa kundi la SPLM Leaders- Former Detainees (SPLM Leaders – FD)
Furaha kwa kila mtu
Katibu Mkuu wa CCM Mheshimiwa Abdulrahman Kinana ambaye alikuwa mwezeshaji wa mazungumzo akisoma dondoo za makubaliano

Meza kuu katika picha ya pamoja na kundi linalojulikana kama SPLM in Government (SPLM-IG)
Picha ya pamoja na kundi la SPLM
in Opposition (SPLM-IO)

Picha na Sekretareti ya mazungumzo hayo
Rais Kikwete na Mzee Malecela wakipongezana baada ya kufanikisha mazungumzo na hatimaye makubaliano ya viongozi wa SPLM
Rais
Kikwete akishukuru vikundi vya ngoma za utamaduni vilivyokuwapo uwanja
wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro kumsindikiza baada ya mkutano wa
mafanikio




0 comments:
Post a Comment