Yesu, kama Bwana, aliwajua watu Zaidi yalivyokuwa
wakijifahamu wao wenyewe. Kuna maelezo mengi katika injili ambapo Yesu
alionyesha kwamba sio tu alijua walichokuwa wakifikiri kwa wakati huo (
soma Marko 2:8)- Yeye alijua historia zao pia ( Yohana 4:18)
Soma Zaburi 139:1-13. Neno la Mungu linatwambia nini hapa?
Kama tulivyoona jana, Yesu alikuwa anayatambua mahitaji ya
watu, na alihudumu kwaajili ya mahitaji hayo, Ki ukweli aliyatambua hata
mahitaji yaliyokuwa chini ya uso wa dunia, ukweli huu unadhirika katika
kisa cha mtu yule aliyekuwa amepooza. Ingawa ilikuwa inaonekana dhahiri
kwamba alihitaji uponyaji wa kimwili, kulikuwa na jambo kubwa Zaidi
pale, ambacho hata kabla ya kumwambia ajitwike godoro lake na kwenda,
“Yesu alisema mwanangu umesamehewa dhambi zako” ( Marko 2:5).
Soma Marko 2:1-12. Ni nini kilichokuwa kinaendelea ndani ya
mwanaume huyu? Ni kwa njia gani hitaji hili la ndani, laweza kuwa
tatizo kwa wale tunao wahudumia?
Yesu alitambua kwamba tatizo pale lilikuwa ni Zaidi ya
ugonjwa. “Hata hivyo haukuwa uponyaji wa kimwili ( kwa yule mwenye
kupooza) alitaka msaada sana katika mzigo wa dhambi. Kama angeweza
kumwona Yesu na kupokea hakikisho la msamaha wa dhambi na kuwa na Amani
na mbingu, Angekubali kuendelea kuishi au kufa. Kwa mujibu wa mapenzi ya
Mungu”-Ellen G.White, The Desire of Ages,uk.267.
Bila shaka sisi hatuwezi kwenda kwa undani kama Yesu
alivyofanya. Hata hivyo tunaweza kuwa na uhakika kwamba wale wote ambao
tunawahudumia, ni viumbe walio haribiwa na dhambi, hiyo ni kusema pamoja
na mahitaji yao mengine wao pia wanahitaji neema ya uhakika, ya maarifa
kwamba yuko Mungu anayewapenda na aliyekufa kwa ajili yao na
anayewatakia yaliyo mema pekee.
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment