Friday, December 09, 2016

 
Mwandishi amejadili pia juu ya yale ambayo mwanadamu yeyote, haidhuru awe katika hali gani, akiyafanya atakuwa na sifa ya kuondolewa katika ulimwengu huu wa adha na kuishi katika ulimwengu usio na hata chembe ya taabu. Kundi linaloishi duniani hata leo bila hofu yoyote ya chochote kwani limewekwa huru.

Pendo Lisilo Kifani inakupatia Muonjo wa Wakati Taabu Itakapokoma.  Kwa kusoma kitabu hiki unawezeshwa kuona japo kwa mtupo wa jicho aina ya maisha katika ulimwengu wa raha usiokuwa hata na chembe ya taabu. Maelezo ya mwandishi yanastaajabisha sana.

Ni shauku kuu ya mwandishi kwamba kwa kukisoma kitabu hiki ujue namna ya kuishi kwa tumaini na amani katika ulimwengu huu wa shida, lakini zaidi kwa kufuata maelekezo yake uwezeshwe kuishi kwa namna ambayo utakuwa na sifa za kuishi katika ulimwengu ule usio na taabu wala shida.

Hiki ni kitabu ambacho kwa hakika kila mwanadamu aliyewahi kupata taabu yoyote anakihitaji sana.  Kwa bei ya shilingi elfu mbili tu utapata nakala hii ya ajabu.  Tafadhali dhihirisha pendo lako kwa wanafamilia na marafiki zako kwa kuwanunulia nakala kila mmoja wao nawe utashangaa jinsi watakavyo neemeka.


Maelezo na
Mchungaji Ezekiah Chaboma.
Meneja usambazaji wa vitabu  

Kanisa la waadventista wa Sabato, Union ya kusini mwa Tanzania.



****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA