Monday, February 25, 2013

Dalili kubwa ya hatua hii ni upele. Vipele huanzia upande mmoja wa mwili na kuenea sehemu zingine za mwili. Vipele hivi hujitokeza kuanzia wakati ambao kidonda kinapokuwa kinapona na vinaendele majuma mengine hata baada ya kidonda kuwa kimepona na vinakuwa haviwashi.
Hatua ya mbali( late stage)
Hatua hii hufuata baada ya hatua hizo hapo juu kuwa zimekwisha. Endapo mgonjwa hakutibiwa huendelea kuw na wadudu kwenye damu hata kama hana dalili. Dalili zake ni kushindwa kutumia viungo, upofu, kufanga ganzi na kupoteza kumbukumbu.
Maambukizi
Kaswende huambukizwa endapo majimaji ya kwenye kidonda hugusana na mwili. Lakini pia huambukizwa kwa njia ya ngono, na hata kunyonya mate na kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Vipimo
Muda mfipi baada ya kupata maambukizi mwili hutengeneza kinga ya kupambana na wadudu wa  kaswende. Hivyo hii kinga inaweza kupimwa maabara kwa kutumia kipimo maalumu. Wakati mwingine uchunguzi huwezwa kufanya kwa kuchukua majimaji kutoka kwenye kidonda.
Uhusiano kati ya kaswende na HIV
Kwakuwa mgonjwa wa kaswende anakuwa na vidonda ni rahisi kupata maambukizi ya HIV.
Matibabu.
Hakuna matibabu ya nyumbani yanayoweza kuponyesha huu ugonjwa. lakini unatibika kwa urahisi kwa kutumia antibiotics amabazo unaandika na  daktari. Hivyo unapokuwa na dalili hizo ni vyema kuwahi hospitali, 
www.masua.blogspot.com

Kaswende hatua ya pili.Ugonjwa wa kaswende unapitia hatua tofauti. Hii ni hatua ya pili. Vipele hivi mara nyingi haviwashi hivyo mgonjwa anaweza asitafute tiba.Hata hivyo ni vyema kutafuta tiba kwani madhara ya kaswende

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA