Siku ya jana ilikuwa ni tukio lililojumuisha furaha,nderemo na vifijo pia bashasha za aina yake kwa kuwekwa wakfu kanisa la kimara na pia hii huonesha jinsi kazi ya Bwana inavyozidi kukuwa na kuenea kwa kasi.
Kuwekwa wakfu kwa kanisa la waadventista wasabato kumewezeshwa na michango ya washiriki wa kanisa na pia kwa ushirikiano na marafiki wa washiriki wa kanisa kwa kutoa kwa moyo michango na kujituma kumefanya kazi hii matunda yake kuonekana sasa,Bwana awabariki sana.
Kuwekwa wakfu kwa kanisa la waadventista wasabato kumewezeshwa na michango ya washiriki wa kanisa na pia kwa ushirikiano na marafiki wa washiriki wa kanisa kwa kutoa kwa moyo michango na kujituma kumefanya kazi hii matunda yake kuonekana sasa,Bwana awabariki sana.
Picha ni Mgeni Rasmi akiwa msafara ambao ni wachungaji na wazee na kanisa la Kimara.. |
Gwaride lililoandaliwa na vijana wa kimara wakielekea walipo Mgeni rasmi na msafara wake.. |
Zoezi la kuvalishwa skafu likafika ambapo kulia ni Mchungaji Letta na kushoto Mchungaji Butoke wakivalishwa skafu hapo jana katika viwanja vya kanisa. |
Zoezi limekamilika na vijana wanarudi kwa ukakamavu .. |
Msafiri akitembea kwa ukakamavu na kuwapa utaratibu Mgeni Rasmi na msafara alioambatana nao siku ya jana. |
Kijana Msafiri mwenye sale ya vijana akiongoza msafara wa Mgeni Rasmi na waliofuatana nao kuelekea katika eneo ambapo shughuli hii inafanyika |
Hatimaye muda ukafika,kijana msafiri akiongoza viongozi na wachungaji hawa katika zoezi la kuweka wakfu kanisa kwa kutoa utaratibu uliokuwa ukifuata.. |
0 comments:
Post a Comment