Tuesday, September 08, 2015

Katika wakati huu ambapo dunia imetawaliwa na mambo mengi maovu yanayosababishwa na mmomonyoko wa maadili katika jamii.
  • Je, elimu uliyopata imekuwezesha kulinda maadili katika jamii? 
  • Je, mazingira ya shule uliyosoma yamekupa msaada kiasi gani kufikia kiwango cha juu cha maadili?
  • Je, unaiandaaje familia na jamii yako kwa ujumla kupata nafasi njema ya kunufaika zaidi au sawa na wewe katika nyanja ya maadili?
Majibu yote ya maswali hayo ni mepesi sana kupatikana kutoka kwa mwanafunzi aliyesoma au anayesoma katika shule ya msingi ya Kongowe.
Ni shule inayomilikiwa na Kanisa la Waadventista Wasabato, inapatikana Kongowe, Kibaha katika mkoa wa Pwani. Inayo madarasa ya awali hadi darasa la saba.

Pamoja na masomo ya kawaida, inafundisha uchaji Mungu, Kujitegemea, Ukakamavu na mengine mengi ambayo yamekuwa ni changamoto katika maadili ya vijana katika jamii.

Hapa tunakuletea matukio katika picha ya baadhi ya wanafunzi wa shule hii, walipotembelea na kuabudu katika kanisa la Waadventisa Wasabato Ilala jijini Dar es Salaam.
Kusanyiko katika Ibada ya pamoja katika Kanisa la Ilala
Baada ya Ibada ya asubuhi, walifanya shughuli ya upimaji afya bure wa Waumini, Pichani ni mmoja ya Wazee wa kanisa akipimwa afya
Mchana walionesha matendo ya ukakamavu na mambo mengine wanayojifunza
Mchungaji wa Vijana hao Emmanuel Rajabu kushoto akihubiri huku akisaidiwa katika kutafsiri kwa lugha ya kiingereza na mkuu wa shule hiyo
Mchana walionesha matendo ya ukakamavu na mambo mengine wanayojifunza
Mchana walionesha matendo ya ukakamavu na mambo mengine wanayojifunza
Mch. Emmanuel Rajabu akisalimiana na watu baada ya ibada
Vijana wadogo, wakisimamia zoezi la upimaji afya
Baadhi ya washiriki wakiwa katika foleni ya kusubiri huduma ya upimaji afya
Waliohudhuria katika ibada ya siku hiyo
Zoezi la upimaji likiendelea, hapo watu wakipima uzito na urefu na zoezi zima likisimamiwa kwa ustadi na vijana wadogo
Katika ibada ya siku hiyo
Moja ya wanafunzi katika shule za awali, akiwa katika tabasamu zito
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

1 comment:

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA