Chuo
Kikuu cha Dodoma kinawatangazia wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga
na Programu Maalumu za Ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati (Special
Diploma in Education Programme) kwa mwaka wa masomo wa 2015/2016 kuwa
wanatakiwa kuthibitisha nia ya
kujiunga na masomo. Ili kudhihilisha na kuhakiki taarifa, wanafunzi
waliochaguliwa wanapaswa kutumia mfumo maalumu wa ki-elekitroniki mahali
palipoandikwa bonyeza hapa. Uthibitisho ufanyike kabla ya tarehe 30/09/2015. Wasiothibitisha kujiunga hawatapokelewa chuoni.
Chuo
kitafunguliwa tarehe 31/10/2015 na fomu za kujiunga zitapatikana kwenye
tovuti ya chuo (www.udom.ac.tz) kabla ya tarehe ya kufungua chuo.
IMETOLEWA NA OFISI YA NAIBU MAKAMU MKUU WA CHUO - TAALUMA, UTAFITI NA USHAURI.
CHUO KIKUU DODOMA.
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment