Tuesday, February 16, 2016

Magreth - mama anayejitambua kama Nabii, ametokea akidai ana ujumbe aliopewa na Mungu kuwaonya wanawake (hasa wakristo) wasivae nguo zinazoonesha uchi bali wavae nguo kama hiyo aliyovaa yeye (pichani kulia). Nilikutana na Magreth alipokuja kwenye semina ya uongozi iliyokuwa inahitimishwa leo hapa Mwenge ili aonane na viongozi wa Konferensi na Union awaambie kile Mungu alichomwagiza kwao. Hapa anajaribu kujibu maswali kutoka kwa mmoja wa wanasemina ndugu Mduma - dereva wa Mwenyekiti wa Union. Magreth ni mwaadventista anayesali huko Kipunguni Ukonga. Ingawa anaonekana kukiamini kwa dhati (conviction) hicho anachokiita mafunuo bado anahitaji msaada ili afahamu asili ya hiyo nguvu iliyo nyuma yake. Tumuombee
 chanzo Stephen Letta


****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA