Waimbaji 14 wa The
Light Bearers toka JCB Studioz za jijini Dar es salaam wameondoka hii
leo Agosti 4,Mwaka huu kuelekea Reading,Uingereza kuimba katika Mkutano
wa Injili wa majuma matatu ambao utaendeshwa na Kanisa la Waadventista
Wa Sabato la Angaza la mjini humo.
Mkutano huo wa Injili utaendeshwa na Mchungaji Baraka Butoke ambaye
aliwahi kuishi na kulelewa na Kanisa la Angaza nchini Uingereza wakati
akiwa kijana mdogo.
Kiongozi wa The Light Bearers Waziri Barnabas ambaye ameongozana na
waimbaji hao amesema safari hiyo ni fursa na nafasi nyingine ambayo
Mungu amewapatia kuhudumu kwa njia ya nyimbo za Injili nje ya mipaka ya
Tanzania.
Kanisa la Angaza limekuwa na utaratibu wa kuwaalika waimbaji toka wa
Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania kwenda kushiriki kwenye
mikutano ya Injili nchini humo kuanzia mwaka 2004.
The Light Bearers mpaka sasa wanamatoleo manne ya audio huku matoleo
mawili yakiwa yanasubiriwa kutambulishwa hivi karibuni katika vyombo vya
habari nchini Tanzania.
Make Money Online : http://ow.ly/KNIC
Make Money Online : http://ow.ly/KNIC
Waimbaji wa The Light Bearers wakiwa katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere muda mfupi kabla ya kuondoka hii leo |
Picha/Habari na Mtangazaji Blog
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment