Somo la Asubuhi linatoka katika kitabu cha MARANATHA,
kitabu ambacho kinadhaminiwa na EGW Writtings maalumu kwa ajili ya
Programu ya IBADA.
Maana njozi hii ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka
ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee;
kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia. Habakuki 2:3.
Imani iliyomtia nguvu Habakuki, watakatifu na wenye haki
siku zile za majaribio magumu ni imani ile ile inayotunza watu wa Mungu
leo. Katika nyakati zilizo na kiza kabisa, katika mazingira yasiyo
mazuri kabisa, Mkristo muumini aweza kudumisha muunganiko kati ya roho
yake na chanzo cha nuru na uwezo. Siku kwa siku, kwa njia ya imani kwa
Mungu, tumaini lake na ujasiri vyaweza kufanywa upya tena.... Katika
huduma kwa ajili ya Mungu hakutakuwa na kukata tamaa, kusitasita, wala
hofu. Bwana atatimiza matarajio ya juu zaidi ya wale wawekao tegemeo lao
kwake. Atawapa hekima inayohitajika kulingana na mahitaji yao
mbalimbali.
Mtume Paulo anatoa ushuhuda juu ya uwepo wa mahitaji kwa
wingi kwa ajili ya roho inayojaribiwa. Yeye alipewa uhakika wa kimbingu,
“Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu.”
Kwa shukrani na ujasiri mtumishi wa Mungu aliyejaribiwa aliitikia: “Basi
nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae
juu yangu. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na
adha na shida, kwa ajili ya Kristo. Kwa maana niwapo dhaifu ndipo nilipo
na nguvu.” 2Kor. 12:9, 10.
Tunapaswa kuiendeleza na kuijenga imani ambayo manabii na
mitume wameishuhudia - imani ambayo anakamata ahadi za Mungu na kusubiri
ukombozi katika wakati aliouamuru na njia aliyoipanga. Neno la hakika
la unabii Iitatimilika mwishoni katika ujio wenye utukufu wa Bwana wetu
na Mwokozi Yesu Kristo, kama Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.
Wakati wa kusubiri waweza kuonekana kuwa mrefu, roho yaweza kuelemewa na
matukio ya kukatisha tamaa, wengi ambao watu wamewaamini waweza
kuanguka; lakini hebu tuungane na nabii aliyediriki kutia moyo Yuda
wakati wa uasi mkubwa sana, kwa kusema, “. . .Bwana yumo ndani ya hekalu
lake takatifu: dunia yote na inyamaze kimya mbele zake.”
Hebu daima tukumbuke ujumbe huu unaochangamsha, “Maana
njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia
mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina
budi kuja, haitakawia. . . mwenye haki ataishi kwa imani yake.”
0 comments:
Post a Comment