Sunday, August 21, 2016

Yesu alishuka kwenye mashua karibu na pwani ya Kapernaumu. (tazama Marko 5) Wanafunzi wake bado walikuwa wamestushwa kutokana na tukio la kukutana na mtu mwenye pepo huko Dekapoli. Kama kawaida, umati wa watu ulikusanyika kumlaki. Wakiwa na shauku ya kutaka kumsikiliza, watu katika umati ule walikuwa wakisukumana ili kuwa karibu Zaidi na Yesu. Mara akaombwa msaada, wakati huu aliombwa msaada na wakuu wa masinagogi.

Soma Marko 5:22-43 Wakati Yesu akiwa njiani kuelekea kumhudumia kiongozi wa sinagogi kitu gani kilimzuia? Na ni kwa jinsi gani alikabiliana na kizuizi hiko? Kitu cha muhimu hapa, Somo gani tunapata hapa kulingana na kisa hiki, kuhusiana na kukabili kizuizi unapokuwa katika kutoa huduma?
Hebu tukabiliane na hili, hakuna kati yetu anayependa kukabiliana na vizuizi, sivyo? Tuna mambo mengi ya kufanya. Sehemu za kwenda, na kazi zinazopaswa kufanyika. Tunaweka malengo kwa ajili yetu na tunahitaji kufikia malengo hayo. Wakati mwingine tunahitaji kufikia malengo hayo kwa muda Fulani tuliojiwekea, hata hivyo vizuizi vyaweza kuingilia kati.

Ndiyo sababu, kama mtu anakuja na haja au ombi la kuhitaji msaada, huweza kuonekana kama vile usumbufu hasa kama wakati sio muafaka. Wakati mwingine unalazimika kutokuacha kile unacho kifanya kwa wakati huo, Ni mara ngapi unapaswa kuacha hicho unachokifanya na kutoa msaada lakini hufanyi hivyo kwasababu hutaki kufanya hivyo?

Hata hivyo mara kadhaa fursa kubwa za kuwahudumia watu wengine mahitaji yao huja na vizuizi. Wengi tunajaribu kuvikwepa vizuizi hivyo na tunasikitika pale mipango yetu inapofutika. Tunapo tazama huduma ya Yesu tunagundua kwamba baadhi ya mahitaji, aliyoyajali mno yalikuja na vizuizi na aliyashughulikia kwa upendo. Tunapofikiri kuhusu hilo, fursa nyingi za kutoa huduma huja kwa njia ya vikwazo. Tumekwisha kutazama kisa cha Msamaria mwema. Nani ajuaye alipokuwa anakwenda na nini alikuwa anakwenda kufanya alipofika pale?, Hata hivyo alisimama na kutoa huduma.

Zungumza juu ya vizuizi.
Mara ya mwisho ili kuwa lini, mtu alikukatiza akiwa na hitaji la kuomba msaada? Uliitikia vipi?

****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA