Somo la Asubuhi linatoka katika kitabu cha MARANATHA,
kitabu ambacho kinadhaminiwa na EGW Writtings maalumu kwa ajili ya
Programu ya IBADA.
Kwa maana, tazama, BWANA anakuja kutoka mahali pake, ili
kuwaadhibu wakaao duniani, kwa sababu ya uovu wao; ardhi nayo itafunua
damu yake, wala haitawafunika tena watu wake waliouawa. Isaya 26:21.
Kwa kasi na tena kwa uhakika hatia inakuja juu ya wakazi wa
miji, kwa sababu ya kuongezeka kwa kudumu kwa uovu utendwao kwa
makusudi. Ufisadi unaotawala, unazidi ule mwanadamu awezao kuuleza kwa
maandishi. Kila siku inakuja pamoja na ufunuo mpya wa ugomvi, rushwa, na
ulaghai; kila siku inakuja na taarifa za kutisha za vurugu na uvunjaji
wa sheria, kutojali mahangaiko ya watu, udhalimu, maangamizi ya kikatiIi
ya uhai wa watu.
Mungu wetu ni Mungu wa rehema. Kwa subira na huruma anadumu
kushughulika na wavunja sheria. . . Mungu anawavumilia sana watu, na
pia miji, huku akiendelea kwa rehema kutoa maonyo ili kuwaokoa kutoka
katika ghadhabu yake; lakini wakati utakuja ambapo sauti yake ya kusihi
itakoma. . .
Hali zinazoendelea katika jamii, hususan katika majiji
makuu ya dunia, zinatangaza kwa sauti kubwa kama radi ya kwamba saa ya
hukumu ya Mungu imekuja na kwamba mwisho wa mambo yote ya kidunia
umekaribia. Tunasimama katika ukingo wa zahama ya karne zote. Kwa haraka
zikifuatana hukumu za Mungu zitashuka - moto, mafuriko, matetemeko,
pamoja na vita na umwagaji wa damu. . .
Dhoruba ya ghadhabu ya Mungu inajikusanya; na watakaopona
ni wale tu watakaoukuwa wamepokea mwaliko wake wa rehema,... na
kutakaswa kwa njia ya utii kwa sheria ya Mtawala wa mbinguni. Wenye haki
pekee watafichwa pamoja na Kristo katika Mungu hadi uharibifu
utakapokuwa umepita. Hebu lugha ya roho na iwe:
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment