Monday, August 22, 2016

Soma Marko 10:46-52 na Yohana 5:1-9. Katika matukio hayo yote, Yesu aliuliza maswali. Kwanini alifanya hivyo?

Zingatia katika matukio hayo yote kwamba Yesu aliuliza walichokuwa wanakihitaji ingawa hitaji lao lilikuwa dhahiri na hata kama sivyo Yesu angelitambua ni nini yaliyokuwa mahitaji yao.
Hata hivyo kwa kuuliza maswali hayo, Yesu alionyesha heshima kwa watu, Alionyesha kwamba alikuwa anawasikiliza, kwamba alijali kuhusu hilo walilokuwa wanakabiliana nalo. Ni masuala mangapi ambayo watu , labda Zaidi ya kitu chochote huhitaji mtu tu wakuzungumza naye, mtu ambaye atawasikiliza? Wakati mwingine kuwa na wazo la kuzungumza juu ya tatizo la mtu inaweza kumsaidia kujisikia vizuri.
 
Fikiria kwa muda mfupi jinsi gani ungejisikia kama ungeingia ofisi ya daktari na daktari akakuangalia mara moj tu na kukuandika dawa na kukutoa nje.Kwa hakika ungekuwa na wasiwasi iwapo mtu huyo alielewa tatizo lako. “Ungeweza sema daktari hakuniuliza mimi, jinsi ninavyo jisikia au hata kusikiliza mapigo ya moyo, wala kupima shinikizo langu la damu au…Mojawapo ya kanuni za utabibu ni kutambua ugonjwa kabla ya kuutibu.”

Dhana hiyo hiyo inatumika katika shughuli za utume wa kitabibu,ambayo hulenga katika ustawi wa watu na afya zao na kuwahudumia katika mahitaji yao kiujumla. Makanisa mengi mno wanafikiri kwamba wanajua ni nini cha kufanya ilikuwahudumia wengine katika jamii yao.Wakati sisi tukijitahidi kuzungumza na watu kuhusu mahitaji yao au mahitaji ya jamii, Huwaonesha kwamba tunajali na hutujulisha sisi kwamba jinsi gani tunaweza kuwatumikia kwanjia ambazo zitakubalika,pia tutatengeneza marafiki wapya.

“Kumbuka kwamba unaweza kuvunja upinzani wowote kwasababu ya maslahi binafsi ya watu unaokutana nao. Kristo alichukulia shauku za wanaume na wanawake alipokua akiishi nao hapa duniani.Popote alipokwenda alikuwa mmsionari na mtabibu.Tunapaswa kwenda huku tukitenda mema, kama alivyotenda. Tumeelekezwa kuwalisha wenye njaa, kuwa visha walio uchi na kuwafariji wenye huzuni”- Ellen G.White, Welfare Ministry.uk 162.
Wengi wetu hatuna tatizo kuelezea maoni yetu.tunawezaje kujifunza kuwa wasikilizaji bora?
 
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA