Friday, August 26, 2016

Soma: Kum. 15:11; Ayu. 29:11-17; Mit.14:31; Mit.19:17;Mdo.3:6;Yak.1-27; Ellen G.White, 

“Pioneering in Australia, “uk.327-338, kwenye kitabu kiitwacho, Welfare Ministry.
Kama ilivyokuwa kwa Yesu Petro alihusika katika kuwafikia wahitaji. Tunaweza kuona mfano huu katika kisa cha Paulo katika vilima vya mars huko Athene. Katika Matendo 17:23, Paulo akiwa amekasirishwa na ibada za sanamu katika mji ule ,Alijiingiza katika mijadala na wasomi na watu wowote katika sehemu ya soko,ambaye angezungumza naye. Aliyatambua mahitaji yao na masuala yao waliyokuwa nayo. Aligundua kwamba wana nafasi kwa Mungu wasiyemfahamu katika maisha yao na kwamba wanahitaji kumfahamu Mungu wa kweli na kuacha kuabudu sanamu zisizo na maana. Kisha akaanza kuhubiri katika masinagogi ambapo wayahudi na “waliokuwa wanamcha Mungu” (Mdo 17:17) Kwa maneno mengine,yeye aliitumia fursa hii ilikuwafikia kiinjili hao waliopo nje, Paulo alitaka kuwafikia huko walipokuwepo, kama tunavyoona jinsi alivyoongea na watu katika sinagogi na watu walioko katika masoko. Umati wa watu uliamini uungu wa aina Fulani kwakuwa walikuwa wamejenga mdhabahu iliyokuwa imeandikwa “kwa Mungu asiyejulikana” (Mdo 17:23).

Na kwa kufanya kazi Paulo alitafuta kuwaelekeza kwa Mungu, “nawahubiri habaru zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua” (Mdo 17:23) Hata hivyo baadae alinukuu mmoja wa washairi,aliyetokea kuandika kitu cha ukweli, “ maana sisi tuwazao wake”( Mdo 17:28). Kwakuanzia mahali watu walipokuwepo alitaka kuwaongoza kutoka katika sanamu zao na kumwelekea Mungu anayeishi na Yesu aliyefufuka kutoka katika wafu. Kwa kifupi, tathimini mahitaji ya wale aliotaka kuwafikia Paulo na kuanzia hapo alijaribu kuwasaidia kutimiza mahitaji yao.
Maswali ya Mjadala
1. “ Yeye ambaye aliwafundisha watu njia ya kupata Amani na furaha , alikuwa pia anawapatia uzito wa mahitaji yao ya kiroho.”- Ellen G.White, The Desire of Ages,uk.365. Ni ujumbe gani wa muhimu tunaopatiwa hapa kwa kuzingatia kwamba tunapaswa kutoa huduma kwa mahitaji ya wengine?

2. Kwanini sisi,tunapokuwa tunafikiri kuwafikia wengine,tunapswa kuwa waangalifu bila kusahau hatma ya lengo letu? Ni nini hatma ya lengo letu? Toa sababu ya jibu lako.

3. Ni kwa namna gani tutajifunza kuona kuwa baadhi ya vikwazo siyo usumbufu ila ni fursa kwaajili ya huduma?Ni kwa vipi Wagalatia 2:20 hutusaidia katika eneo hili?
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA