Soma Matendo 9:36-42. Ni nini alichokifanya Dorkasi kule
Yafa baada ya kugundua kwamba amezingirwa na wahitaji? Katika Matendo
9:41, Ni nini maana ya kifungu hiki cha maneno, “wanaoamini hasa
wajane”?
Dorkasi alikuwa mwanafunzi wa vitendo, “ Katika Yafa
kulikua na mwanafunzi mmoja aliyeitwa Tabitha.” (Matendo 9:36). Inaweza
kusemwa, ”kwamba katika ( jina la mji wako) kuna wanafunzi ( taja majina
yao) ambao wamejawa na “matendo mema na tabia njema” Mdo. 9:36.
“Waaminio” ni washiriki wa kanisa la Kikristo; “wajane” ni
pamoja na washiriki wa kanisa na wale ambao sio washiriki. Dorkasi
aliwahudumia wote. Yafa yako inapaswa kuwa nje na ndani ya kanisa lako,
kujali kwa uthabiti wale walio ndani ya kanisa pia ni uinjilisti wenye
nguvu(soma Mdo. 2:42-47). Watu nje wanaweza kusema tazama jinsi hao
Waadventsta Wasabato walivyo na upendo na kujali.
Soma Yohana 13:34-35 na Yohana 15:12. Ni nini ujumbe
unaopatikana katika maandiko hayo matatu, ni kwanini ni muhimu kwetu
kama kanisa kufuata? Ni kwanini wakati mwingine inakuwa ngumu kufuata
kwa bidii?
Wakati mipango ya kuwatumikia wa nje ya kanisa lako,unapaswa kufikiria mtindo,mbinu ambayo utatumia.
Amy Sherman anaelezea mitindo mitatu, ambayo kanisa
linaweza kutumia katika kuhudumia jamii. Mtindo wa kwanza : mtindo wa
Mkazi unalenga katika kukidhi mahitaji ya jamii iliyo karibu kabisa na
kanisa lako. Mwanamke aliyekuwa akitoa huduma kwa waathirika wa UKIMWI
Alichagua jamii iliyomzunguka “ Yaffa”
Mtindo wa pili, Mtunza Bustani, Mtindo huu humaanisha
kuendeleza huduma inayofungamana na maeneo jirani nje ya kanisa lako
Kama mtunza bustani anavyoona bustani ni ongezeko tu la nyumba yao,
wakati mwingine makanisa kadhaa huungana kuendesha kituo cha huduma kwa
jamii nje ya kila jamii inayowazunguka. Katika Mji mmoja makanisa kadhaa
wanaendesha huduma ya kuhifadhi vyakula bora, kutokana na mradi huu
wameanzisha kanisa lingine jipya.
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment