Thursday, August 25, 2016

“Mkabidhi BWANA kazi zako na mawazo yako yatathibitika” Mithali 16:3 

Mara kanisa lako linapokuwa na maono thabiti ya jinsi linavyoweza kuhudumia jamii ni muhimu kuendeleza mpango huo ambapo idara zote za kanisa zinweza kufanya kazi ili kufanya maono yao yawe ya kweli, Ingawa unaweza ukajiona wewe sio kiongozi katika kanisa lako, lakini unaweza ukachangia. Pia ni vizuri kwa washiriki wote wa kanisa kuelewa mchakato huu, kwakuwa hili linahusu utume wa kanisa lako kwa jamii.

Kimsingi, mpango mkakati wa kanisa unapaswa kuzingatia angalau vyanzo vitatu 1: Nyenzo kutoka katika kanuni ya Biblia na Roho ya unabii 2: Maarifa ya kutambua mahitaji ya kijamii 3: Nyenzo kutoka katika kwa washiriki. Baadhi ya makanisa yamekusanya nyenzo mbalimbali kutoka kwa washiriki kwa kupitia tafakuri zao, wakati wanapoalikwa kutoa mawazo yao,njozi zao kwaajili ya kuwafikia watu wanje na kuboresha hali zao ndani ya kanisa.

Soma Luka 14:25-35. Je kifungu hiki cha maneno kinahusikaje kikamilifu na mipango inayohitajiwa ili kutimiza utume wa kanisa lako?
Kama unafikiria kuhusu mchakato unaohitajika ili kukudhi mahitaji ya jamii yako kwa ufanisi, Unaweza kufikiri: Hili linachukua uthabiti pamoja na muda. Tungependelea kupitia njia mkato. Mifano miwili inatonya dhidi ya kuchukua majukumu ya utume na uanafunzi kwa wepesi.

 Hutukumbusha kwamba uchambuzi na mipango wa utume wetu ni vya muhimu. Ni suala la uwakili mwema, ladha ya chumvi katika Luka 14:34, Huwakilisha ibada. Bila hili, huduma yetu, uanafunzi wetu ni bure na hauna maana. Tunahitaji kuwa na bidii katika ibada kamilifu na Imani kwa Bwana wetu, na kama tunayo hiyo bidii na ibada kamilifu huduma pia itafuata.
Je, Ni njia gani ambazo unaweza kufanya Zaidi pamoja na kanisa lako katika kuandaa na kupanga mapema kabla ya kuifikia jamii huko nje?
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA