Saturday, September 24, 2016

Dr. Taphinez Machibya

Na Dr. Taphinez Machibya

MFUMO WA KINGA MWILINI: Ni ukweli ulio dhahiri kwamba kwa  msaada wa Mungu, mwili unaweza kujiponya wenyewe.

Kama vile mwili ulivyo na uwezo wa kukitumia chakula tulacho ili kuweza kuupatia mwili nguvu,joto, ukuaji na urekebishwaji vivyo hivyo Mwili unazo njia ndani yake za kuleta uponyaji mara tu mtu apatapo ugonjwa . Natural Remedies Encyclopedia:Basic Principles of Healing.pg.18

Ni kwa nguvu ya Mungu pekee inayoweza kutufanya na kutuweka salama. Hakika, ni Mungu ambaye siyo tu alituumba, bali ndiye yeye pia ambaye aliumba vyakula tunavyo hitaji!  Natural Remedies Encyclopedia:Basic Principles of Healing.pg.18

 Mfumo wa mwili daima hukabiliwa na kuharibika na kuchakaa. Lakini kuna njia ndani ya mwili ambazo hufanya kazi katika kusafisha, kurekebesha na kutengenza. Badala ya kutumia nishati na virutubisho kutoka chakula tulacho katika kumeng’enya chakula na katika misuli n.k, mwili huelekeza matumizi yake kwa ajili ya kusafisha, kurekebesha, na kujenga upya.  - Natural Remedies Encyclopedia:Basic Principles of Healing.pg.18

  Kazi hii ya usafishaji, urekebeshwaji na kujenga upya,hufanywa kupitia mfumo wa kinga mwilini.

  Mara mtu anapokuwa mgonjwa, chembechembe hai, viungo, tishu na mifumo ya mwili huwa chakavu na zilizojawa uchafu na sumu.

  Neno ugonjwa hutafisiriwa toka neno la kiingereza “Dis-Ease” Ambayo humaanisha mwili “kutokuwa-SawaSawa” - Natural Remedies Encyclopedia:Basic Principles of  Healing.pg.18

  Hivyo ugonjwa na dalili zake huwa ni matokeo ya asili (nature) katika kuusafisha, kuurekebesha na kuujenga upwa mwili(Healing Crisis).

  Dalili za ugonjwa kama homa,kukohoa, kuchoka mwili, vipele na majipu, kutokwa jasho, kupoteza hamu ya kula, usingizi sana, kutapika na kuharisha n.k, vyote hivi huwa ni sehemu ya uponyaji (Healing Crisis).

  Matabibu na watu wakawaida wamekuwa wakiifahamu hali hii kwa miaka maelfu. - Natural Remedies Encyclopedia:Basic Principles of Healing.pg.18



KINGA YA MWILI :

Ni mkusanyiko wa wa chemchembe hai, tishu na ogani za mwili ambazo huungana pamoja katika kuukinga, kuukarabati na kuujenga upwa mwili dhidi ya ajari, uchafu, sumu au maambukizi ya wadudu mwilini.

Mwili hupambana na yote hayo:

  Kwa kuwa na uwezo wa kuzitambua  hatari/adui (Antingens)zozote mwilini kama vile: uchafu,sumu,wadudu (bakteria, virusi,fangasi, minyoo na parasaittari na kuzitoi wowote),na Chembechembe hai ama tishu zilizo haribika Mf:Chembechembe hai za kansa.

  Kwa kuwa na uwezo wa kuzitofautisha chembechembe hai , tishu na viungo vya mwili vilivyo salama. (National Institute of Allergy and Infectious Diseases: Immune System MSD Manual, Consumer Version:Overview of Immmune System)
 



****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA