Na Dr. Taphinez Machibya |
.
MAANA.
• Kuhara maana yake ni kuharisha au
kupitisha kinyesi chenye damu.
• Hutokea hasa wa watoto chini ya
miaka mitanoi
• Kinyesi chaweza uwa na damu nyingi
au kidogo au nyingi au kuwa na vitu kama kamasi kamasi hivi.
TAKWIMU:
• Magonjwa ya kuhara ni ya pili
katika uuaji wa watoto duniani kote.
• Shirika la afya duniani WHO,
linaonesha kila mwaka zaidi ya watoto 700,000 wenye umri chini ya miaka 5 hufa
kwa magonjwa ya kuhara.
• Magonjwa haya yanazuilika kwa njia
mbalimbali.
SABABU ZA
KUHARA
• Maambukizi ya vimelea kama bacteria
(e.coli, shigella, etc), virusi (rotavirus)na protozoa(entamoeba histolytica,
Giardiasis, B. coli).
• Magonjwa kama ukimwi
• Utapiamlo
• Magonjwa ya UTI,
• Baadhi ya madawa
UENEAJI NA
MAAMBUKIZI.
• Magonjwa ya kuhara yako ya aina
nyingi, mengine siyo ambukizi lakini mengine ni ya kuambukiza .
• Mfano ni homa ya Matumbo(Typhoid
fever), kipindupindu (Cholera), kuhara damu (dysentery) ,minyoo aina mbalimbali
n.k
• Magonjwa haya husambaa kwa ulaji wa
kinyesi kwa njia tofauti,kama vile:
Ø Kula chakula bila kuosha mikono
Ø Kunywa maji yasiyo salama
(chemshwa)
Ø Nzi,mende na wadudu wengine kutua
kwenye kinyesi kisha kutembelea chakula
Ø Kunyonya vidole visivyo safi n.k
Ø Chupa za kunyonyeshea zisizo fanyiwa usafi au matiti ya mama yasiyo safi.
TABIA ZA
WADUDU WA MAGONJWA YA KUHARA.
• Kufahamu tabia za wadudu wa kuhara
husaidia kuelewa jinsi ya kujikinga na kukinga watoto dhidi ya magonjwa.
• Wadudu wengi wa magonjwa ya kuhara
huwa na tabia zifuatazo;
ü Hawaonekani kwa macho
ü Huweza kukaa kwenye chakula na
mabaki ya chakula bila kufa zaidi ya siku 4, hukaa kwenye maji zaidi ya siku
11, na kwenye kinyesi ama nguo au nepi zenye kinyesi kwa zaidi wiki 7.
ü Hubebwa na kusambazwa kirahisi na
nzi,mende n.k
ü Huzaliana kwa haraka sana (ndani
ya masaa machache wadudu huweza kuwa mamilioni)
ü Hufa kwa joto la juu kuanzia 60 C ,
ama kwa madini ya Chlorine.
JINSI YA
KUWALINDA WATOTO NA WANAFAMILIA.
• Matumizi sahihi ya vyoo. Kinyesi
cha wanafamilia rika zote hata watoto kitupwe kwa usahihi chooni.
• Vyoo vifanyiwe usafi na kupigwa
dawa (fumigation) kuondoa nzi, mende, na wadudu watambaao na kuruka wanaoweza
kusambaza magonjwa.
• Kila mwanafamilia kuosha mikono
kila baada ya kutumia choo, na kabla ya kuandaa chakula ama baada ya kula.
• Kuhifadhi chakula sehemu salama na
safi
• Kupasha chakula vizuri kabla ya
kutumia
• Kutumia maji safi na salama kwa
kunywa, kutengenezea juisi, kusafishia ,matunda na mboga zinazoliwa zikiwa
mbichi, kuosha chupa za chakula cha mtoto.
• Maji safi hufanywa kuwa salama kwa
kuchemshwa hadi kutokota ama kuweka madini ya chlorine.
• Kunyonyesha bila kuchanganya na
chakula kwa miezi 6 ya kwanza ya mtoto,Maziwa ya mama yana kinga dhidi ya
baadhi ya magonjwa, Maziwa haya kwa miezi 6 ya kwanza ni lishe kamili na
toshelezi kwa mtoto.
• Kuwapatia watoto lishe ama mlo
kamili wenye Protini, wanga , vitamini ,mafuta, madini na nyuzinyuzi. Lishe
bora huongeza kinga ya mtoto kwa magonjwa ambukizi.
• Kuhudhuria kliniki na kuhakikisha
mtoto anapata chanjo zote stahiki kadri
ya umri wa miaka 5.
NINI
KIFANYIKE MTOTO ANAPOHARISHA?
• Tafuta kumwona daktari mapema
iwezekanavyo , mtoto akihara zaidi ya mara 3 kwa siku 1,ama ukiona damu ama
makamasi kwenye kinyesi.
• Mtoto anayehara na kutapika
aharakishwe zaidi hospitali.
• Wakati ukitafuta msaada wa daktari
hakikisha mtoto hapungukiwi maji mwilini kwa kumpatia ORS na chakula kama
kawaida.
• Usimpatie mtoto dawa yoyote bila
ushauri wa daktari.
• Msafishe mtoto vizuri kwa maji safi
na sabuni kila anapohara na kutupa kinyesi chake vizuri chooni ,nepi zenye
kinyesi zinaweza kulowekwa na jiki na kusafishwa kwa sabuni.
UNAPOFIKA
KWA DAKTARI:
• Uwe na taarifa sahihi juu ya ;
Ø Lini ama saa ngapi mtoto alianza
kuhara.
Ø Kama anahara na kutapika
Ø Amehara na kutapika mara ngapi
Ø Kinyesi chake kinafananaje
Ø Amepatiwa huduma gani ya kwanza
Ø Kama yuko kwenye dawa yoyote
Ø Kama ametoka kupokea chanjo yoyote
siku za karibu.
HITIMISHO:
Kuwalinda watoto wetu na familia zetu dhidi ya
magonjwa ambukizi ya KUHARA ni jukumu letu sote. Tutimize wajibu wetu wa
kupigana na magonjwa haya,ushindi ni hakika tukifuata taratibu bora za afya!
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment