Friday, October 07, 2016


Na Dr. Taphinez  Machibya


 .


Kila jambo lina utaratibu na kanuni zake ili liweze kuwa na matokeo chanya maishani. Vivyo hivyo hata mwili wa binadamu una kanuni zake na hivyo ili tuweze kupata manufaa ya chakula hasa baada ya mlo, yatupasa kuzingatia yafuatayo;

1.       USILE MATUNDA MARA TU BAADA YA KULA: Hii husababisha tumbo kujaa gesi /hewa ambayo huingilia mmeng’enyo wa chakula. Kula matunda saa 1-2 kabla au baada ya kula.



2.       USINYWE CHAI: Kemikali ya Asidi iliyomo katika chai husababisha chakula kugandamana na kushindwa kusharabiwa vema katika kuta za utumbo



3.       USILEGEZE MKANDA( WA NGUO): Hii inaweza kusababisha utumbo kusokotana , kupandana na  kuzibwa kwa njia ya chakula.





4.       USIOGE : Hii itapelekea damu kwenda sehemu za mbali za mwili ili kusawazisha joto vema kama vile mikononi,miguuni,na sehemu zingine za mwili hivyo kudhoofisha umeng’enyaji na wa chakula na uchukuliwaji wa virutubisho vya chakula katika utumbo.



5.       USITEMBEE UMBALI MREFU/KUFANYA KAZI NZITO /MAZOEZI : Hii husababisha mfumo wa mmeng’enyo wa chakula kushindwa kufyonza virutubisho toka tumboni kwa sababu ya mvurugano wa shughuli zinazofanywa  na mhusika.





6.       USIVUTE SIGARA: Kwa sababu mwili unafyonza chakula wakati huu,utafiti unaonyesha kwamba kuvuta sigara moja (1) baada ya kula ni sawa na mtu aliyevuta sigara 10,hivyo kuongeza uwezekano mkubwa wa kupata magonjwa ya kansa haraka zaidi.



7.       USILALE MAPEMA: Kulala mara tu baada ya kula hubana misuli ya tumbo na kuzuia chakula kisitembee sawia tumboni,hii hupelekea maambukizi na magonjwa ya tumbo na utumbo kwa sababu chakula huishia kuozea tumboni na kuruhusu wadudu wa magonjwa mbalimbali kustawi vema.



Hivyo ili tuweze kula kwa faida na chakula kiwe cha manufaa mwilini baada ya kuliwa ni vema tukiyazingatia hayo!



****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA