Saturday, December 24, 2016


Halikuwa kusudi lake Kristo kubadili, kuondoa, kutangua, wala kuibatilisha sehemu yo yote ya sheria  hii.     "Msidhani  ya  kuwa  nalikuja  kuitangua  torati  au  manabii;     la,  sikuja  kutangua,  bali kutimiliza." (Mathayo 5:l7).

Badala  ya  kuitolea  sheria  hiyo  sifa  mbaya,  Kristo  alikuja  kuifanya  iadhimishwe.     "BWANA
akapendezwa kwa ajili ya haki yake, kuitukuza sheria na kuiadhimisha." (Isaya 42:21).

Naam, kwa kadiri Sabato inavyohusika, Kristo aliitunza, pamoja na kila amri nyingineyo.   "Siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake." (Luka 4:l6).

Kusema kweli, imani kwa Kristo, badala ya kuiweka sheria kando, inaithibitisha na kuiimarisha. "Basi,  je!    twaibatilisha  sheria kwa imani hiyo?    Hasha!    kinyume cha hayo twaithibitisha sheria." (Warumi 3:3l).

Sheria  hii ya Mungu, ambayo ndani yake imo amri ya Sabato, inatangazwa na Paulo kuwa ni "ya rohoni," "takatifu,"   "ya haki,"     na "njema."   "Kwa maana twajua ya kuwa torati [sheria] asili yake  ni  ya  rohoni"  (Warumi  7:l4).    "Basi  torati  [sheria]  ni  takatifu,  na  ile  amri  ni  takatifu,  na  ya haki, na njema." (Warumi 7:l2).

Sheria hii ni lazima ishikwe kama sharti la kupata uzima wa milele.   "Heri wale wazishikao  amri zake, wawe na haki kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake."    (Ufunuo
22:l4, Tafsiri ya King James Version).

Naam,  hiyo  ndiyo  kanuni,  au  kipimo,  ambayo  kwayo  ulimwengu  wote  utahukumiwa.    "Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru." (Yakobo 2:l2).




****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories:

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA