Thursday, December 22, 2016


💔Dhambi  ilikata  mawasiliano  kati ya Mungu na mwanadamu, lakini kwa upendo  wake  Mungu  alitafuta  njia nyingine ya mawasiliano.     “Kisha akawaambia,  Sikilizeni  basi  maneno yangu; akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono, nitasema naye katika ndoto” (Hes.12:6). Nabii akiwa katika maono macho yake yanatazama na kuona mambo ambayo Mungu anamwonesha; watu wengine walio karibu naye hawawezi kuona mambo hayo; waweza kusikia sauti au tetemeko (Dan.10:7; Mdo.9:3-7).   Ndoto huja usiku anapolala; anaoneshwa mambo fulani muhimu anayopaswa kuwaambia watu wa Mungu au kuwaonya mataifa. Wakati mwingine Mungu anamtuma malaika wake na ujumbe maalumu kwa nabii (Dan.9:20-23; Ufu.19:9,10)

💝Mungu hawezi kuliangamiza taifa lo lote bila kuwasiliana na manabii wake ile watoe onyo mapema kusudi watu wale wajirekebishe nyendo  zao.     “Hakika Bwana Mungu hatafanya neon lo lote bilz kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake”  (Amosi  3:7).  Nuhu,  Ibrahimu  na Yona walipewa ujumbe maalumu wa maangamizi   ya   wanadamu   na   walitoa onyo.   Waliojirekebisha hawakuangamizwa; wale waliokataa kujirekebisha   waliangamizwa   (Yer.18:7-10; Mwanzo Sura ya 18 na 19; Yuda 7; 2 Pet.2:6; Yona 3 hadi 4:1). Dunia hii ya sasa inafanana na Sodoma na Gomora na manabii wanatupasha habari kuwa itateketezwa kwa moto kama Sodoma na Gomora (2 Pet.3:1-7,10).

Kwa   kuwa   sisi   ni   watu   wa kawaida,    hatujui    Mungu    anakusudia
kufanya  nini  hapa  duniani,  ni  jambo  la muhimu mno kuwasikiliza manabii wake. “Angalieni  msimkatae  yeye  anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa   yeye   aliyewaonya   juu   ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni” (Ebr.12:25,26). Mungu ndiye anayewapasha habari za matukio duniani manabii wake. Hivyo tutapata hasara sisi wenyewe tukiwapuuzia, wala hatutafanikiwa katika safari yetu ya mbinguni.  “…mwaminini  BWANA, Mungu wenu, ndivyo mtakavyothibitika; waaminini manabii wake, ndivyo mtakavyofanikiwa” (2 Nya.20:20).

🛐 Haitoshi kujihami na kusema kila nabii anayekuja ni nabii wa uongo maana
manabii wa kweli wapo pia hadi mwisho wa dunia (1 Kor.12:28; Efe.4:8,11-14).  Je, kanisa limefikia umoja wa imani sasa? Hapana.    Je,  kanisa  limefikia  cheo  cha kuwa na tabia kama ile ya Yesu?  Hapana. Je, waumini wanamfahamu sana Yesu? Hapana.    Kwa ajili hiyo tunawahitaji manabii na wahudumu wengine kutoa huduma yao ndani ya kanisa la Mungu.

📢 Unabii wa Yoeli 2:28-32 ulitimia kwa sehemu tu siku ile ya Pentekoste (Mdo.2:17-21). Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste ni “mvua ya vuli.”     Tunangojea  “mvua  ya  masika” Roho Mtakatifu atakapomwagwa tena itakapotangazwa Amri ya Jumapili kwa ulimwengu mzima na kulazimishwa (Ufu.13:16,17; 18:1-4). Uwezo wa Roho Mtakatifu utakuwa mara kumi kuliko ule wa Pentekoste na watu wa Mungu waliodanganywa watarudi katika zizi la Kristo (Ufu.18:4; Yn.10:16).
Ni  kweli  Yesu  alionya,  akisema, “Jihadharini  na  manabii  wa  uongo,  watu
wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini  kwa  ndani  ni mbwa-mwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao” (Mt.7:15,16). Wamo ndani ya makanisa, wanatumia  jina  la  Yesu,  lakini wametumwa na Shetani kuwadanganya wateule ili wapotee na kujitenga mbali na Mungu (1 Kor.11:13-15; Yer.14:14:16; Mt.24:11,24; 7:15-23). Habari njema ni kwamba   tutawatambua.      Viko   vipimo vikuu vinne vya kuwapima manabii kama wametumwa na Mungu au na Shetani. Lazima nabii atimize vyote vinne, akishindwa kimoja hafai.
 🔷Kipimo Cha Kwanza:
     
Sheria na Ushuhuda  (Isa.8:20).  Wapimwe  kwa Amri Kumi za Mungu, pia mafundisho yao yapimwe kwa Biblia. “Na waende kwa Sheria   na   Ushuhuda; ;   ikiwa   hawasemi sawasawa na neon hili, bila shaka kwa hao hapana   asubuhi”   (Isa.8:20).   Wakivunja moja tu wamevunja zote (Yak.2:10-12). Karibu zaidi ya asilimia tisini na tano ya manabii watatupwa mbali kwa kipimo hiki peke yake; hata mtu asiyeijua Biblia anaweza kuwapima bila shida. Kwa vile Amri za Mungu zimebadilishwa, hapa nanukuu kama zilivyotangazwa mlimani Sinai:

1⃣ Usiwe na miungu mingine ila Mimi.

2⃣ Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha  nne  cha  wanichukiao,  nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.


3⃣ Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.

4⃣ Ikumbuke siku ya sabato uitakase. Siku sita  fanya  kazi,  utende  mambo  yako  yote; lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA, Mungu  wako,  siku  hiyo  usifanye  kazi  yo yote,  wewe, wala mwana  wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa. 

5⃣ Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.

6⃣ Usiue. 

7⃣ Usizini.

8⃣ Usiibe.

9⃣ Usimshuhudie jirani yako uongo.

🔟 Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.

Manabii wengi       wanaojitapa Kipimo hiki tu kinawatupa nje
🔷Kipimo cha Pili: 

Matunda au Maisha yao (Mt.7:20).  “Ndiposa  kwa  matunda  yao mtawatambua”  (Mt.7:20).  Hiki  si  rahisi mpaka  uwe  umekaa  na  nabii  huyo  kwa kipindi fulani na kujua tabia yake. Lakini yaliyo   moyoni   mwa   mtu   mara   nyingi yanatoka  kinywani  mwake  na  kudokeza tabia yake.  Pia mafundisho yake yapimwe kama  yanawafanya  watu  wamjue  Yesu zaidi au yanawapeleka mbali naye. Maisha ya anasa ulevi na mambo ya ajabu hutayasikia katika maisha yake daima hutafuta utukufu wa Mungu sio wa kwake.

♦Kipimo cha Tatu: 

Kukubali kuwa Yesu alikuwa na mwili kama wetu (1 Yoh.4:1-3).
 “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi   wametokea   duniani.   Katika   hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo   kwamba   Yesu   Kristo   amekuja
katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu.
Na   hii   ndiyo   roho   ya   Mpinga   Kisto ambayo   mmesikia   kwamba   yaja...”   (1
Yoh.4:1-3). Yesu asingetusaidia kitu kama angekuwa na mwili tofauti na wetu, maana angetumia   nguvu   za   Mungu   kushinda majaribu.  Habari  njema  ni  kwamba alikuwa na mwili kama wetu, hivyo anaweza kutusaidia (Ebr.2:14-18; 4:14-16; Yn.1:1-3,10,14).
 
 🔷Kipimo cha Nne:
 Unabii Uliotimia (Yer.28:9).   “Nabii   atabiriye   habari   za amani, neno la nabii yule litakapotokea, ndipo nabii yule atakapojulikana, kuwa BWANA amemtuma kweli kweli” (Yer.28:9). Lakini tahadhari kubwa! “Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia,  akisema,  Na  tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto; kwa kuwa BWANA,   Mungu   wenu,   yuawajaribu, apate  kujua  kwamba  mwampenda BWANA, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote…” (Kum.13:1-11). 

🌹🌹Tumeona manabii wengi wakiwatabiria maraisi mbalimbali na unabii wao haukutimia, wengine wanatabiria vifo wengine, na mambo mengi ya ajabu tunayoendelelea kuyaona sasa🌹🌹

👉🏾ZINGATIA:
Kufanya miujiza kwa jina la Yesu sio kithibitisho cha unabii maana hata manabii wa uongo hufanya miujiza

🔷Mathayo 7:21-23 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

🔷Ufunuo 13:13 Naye afanya ishara kubwa, hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu.

📢♦Usiwaogope  manabii  au  mitume, wapime kwa vipimo     hivyo vinne, utawatambua walio wa kweli na wa uongo♦📢


****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA