Waimbaji wa kikundi cha Yu hai |
Kikundi cha yu hai
kilianzishwa rasmi mnamo tarehe 25/08/2013 katika shule ya Pugu sekondari kikiwa
na waimbaji watano, ambao ni Godson Athumani sauti ya nne, Severine Mlungwana sauti ya nne, Paul Elias sauti ya
tatu, Yoel E. ndegea sauti ya pili na
Enock Zabron sauti ya kwanza
JINA LA KIKUNDI:
Tarehe 25/08/2013
ndipo jina la kikundi lilipatikana ‘YU HAI’ kutoka katika majina matatu ambayo
yalikuwa yamependekezwa, majina hayo ni sauti ya uamsho, nyota ya asubuhi na yu
hai ambalo ndilo lilipitishwa.
Hakika MUNGU mwenyewe alichagua jina hilo, baada ya hoja nyingi kuhusu majina
yaliyokuwa yamependekezwa, tulipiga magoti na kuomba ili MUNGU mwenyewe
achague, mwenyekiti Godson alifumba macho baada ya ombi lile na kuchukua
karatasi mojawapo kwa imani kuwa jina hilo ndilo litakalotumika maana MUNGU
amelikubali. Hapo ndipo jina la kikundi lilipoanza kutumika rasmi. Jina la BWANA LITUKUZWE.
Inaendeleaa..........
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment