Monday, January 23, 2017


1Yohana 4:7-8 "Wapenzi, na tupendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo. 

Kati ya mambo ambayo shetani ameyatumia vibaya ili kuwanasa, na kuwajeruhi wengi ni neno UPENDO. Shetani ameharibu akili za vijana na wazee kwa kutumia neno hili upendo, wengi wameshindwa kujua tofauti kati ya upendo wa kweeli na tamaa ya macho au mwili. Mtu akiambiwa NAKUPENDA, nati zote za mwili zinalegea, bila hata kujua nini kinafuata.

Wengi wamepitia maumivu yasiyoisha, hadi kufikia kujijutia nafsi, kwa sababu tu ya kuukubali upendo feki wa tamaa za ngono, uliokuja kama upendo wa kweli. Vijana wengi wanaanzisha uchumba wa kichina (Feki), na unaishia kwa kuumizana, bila kusahau ndoa zinazogeuka ndoano, yote ni kwa sababu ya kutojua maana sahihi ya Upendo unaoanzisha mahusiano.  

Utasikia kijana anasema; "Naamini hunipendi" eti sababu kakataliwa Ngono. Hivyo tafsiri ya shetani ya neno Upendo au kupenda kwa watu wa jinsia tofauti ni kutimiza tamaa za Mahaba au kudunguana maembe, wakati tafsiri ya Mungu ni kutii AMRI za Mungu ikiwemo ya "USIZINI" au kuwa na tabia ya Mungu - 2Yohana 1:6.

Hebu kila mmoja ajihoji, ni upendo gani uliowaunganisha? au ni upendo gani unaoendelea kati yao? Nani anautawala, ni Mungu au yule mzee wa mkuzimu? Mahusiano yako na huyo unayemwita sweteee au mchumba au hawala, boy friend, babeee au yeyote unayeishi naye na kufanya naye ngono, NJE AU KABLA YA NDOA HALALI, unafikiri mwisho wake ni upi? Usidanganyike huo ni mtego na umeshanasa. 

Bado mlango wa wokovu wa kweli ungali wazi, vijana kwa wazee wanaalikwa kuingia, kwa maana usiku umeendelea sana na pambazuko la kheri liko karibu. Bado tumaini la kumshinda shetani lipo kwa wote wanaosalimisha maisha yao kwa Mwokozi. 

Mtajeruhiwa na muovu shetani hata lini? kujiita, mkristo, nimeokoka, mpendwa, mcha Mungu, mwimbaji, nambii, mtumishi na kuhudhuria kila huduma za ibada na maombi, havina maana kama mkuu wa giza ndiye anayetawala maisha. 

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE KUJAA WEMA WA MUNGU

Na: Ev. Eliezer Mwangosi 
Mawasiliano: 0767 210 299 - WhatsApp - 0766 99 22 65
Utabarikiwa ukiwasambazia wengine ujumbe huu. 



****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
Categories: ,

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA