Fikiria juu ya michezo ya kama;
=Mpira wa aina zote na namna unavyochezwa
=Ulimbwende ambapo watu hushindanishwa wakiwa nusu uchi
=Miziki ambapo watu hucheza wakiwa na mavazi ya ajabu sanaaaa ama huimba nyimbo ambazo humghadhabisha MUNGU
HISTORIA YA MPIRA:
Mpira
ulianza mwaka 1863 mwezi 10, walikuwepo watu kadhaa waliotoka katika
shule kadhaa uingereza na club chache zilizokuwapo hapo, wakawa
wamewakilisha vikundi 11 na ndio wakakusanyika mwezi 10,1863 na kuanza
kutunga sheria za kupatana za mchezo.
Hawa
ndio waliosababisha kiundwe chama cha mpira ambacho kinaitwa FA
(FOOTBALL ASSOCIATION) cha England mwaka huu 1863 ambao ni mwaka wa
karibuni sana Baada ya Kristo.
USHABIKI WA MPIRA NI KUSHABIKIA SHETANI
Kama
tulivyoona tafakari pale mwanzo, hivi wawezaje shabikia watu kufukuza
mpira na ukawa na midadi na ushabiki wa juu kabisa hadi kufikia
kujinyonga endapo Timu yako imefungwa pasipo misingi ya ushetani? “ Ni
rahisi sana mtu kufa kwa ushabiki wa mpira wa miguu kuliko kufa kwa
kumtetea Mungu wake”,
DONDOO KUDHIHIRISHA MPIRA NI MPANGO WA SHETANI
(i)
Shetani kajiwekeza zaidi katika anasa/starehe na ambazo binadamu
hupenda(Uzinzi,ulevi,mpira) ili kuwavuta wa wanadamu.Starehe za kidunia
ni mali za shetani na anafanya hayo kurecruit wafuasi.Ni rahisi sana
kukesha unaangalia mpira au mapambano ya ngumi kuliko kukesha
ukiswali/kusali katika mkesha.Ni rahisi sana kutoa ofa ya mpira kwa
mashabiki kuliko kutoa futari mwezi mtukufu.
(ii)
(WAKOLOSAI 3:17) “KILA MFANYALO KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI LOTE KWA
JINA LA BWANA YESU NA KUMSHUKURU MUNGU BABA“Ni muhimu kuelewa ndani
yetu tuliokoka kuna mafuta au tuna dhamiri ambayo inatufundisha kujua
mema na mabaya (1PET2:26-27).Hata kama jambo hatujajifunza kwa undani
juu ya jambo fulani,ndani yetu kutakuwepo roho mtakatifu akitufundisha
kuwa hapa siyo na hapa ndiyo.
Sasa
kila tunalolifanya kwa neno au kwa tendo, anasema tulifanye hayo yote
kwa kufungua kwamaombi.sasa kutokan na mafuta ndani yetu JE TUNAWEZA
KUFUNGUA MECHI YA MPIRA KWA KUSHUKURU BABA KWA MAOMBI? Utaona ndani yetu
inakataa.
(iii) (YOHANA
5:19) “MWANA HAWEZI KUTENDA NENO MWENYEWE ISIPOKUWA AMEMUONA BABA
ANALITENDA”. (YOH 14:6-9) Hivyo hatuna budi kujiuliza kutokana na maisha
ya YESU, JE INAWEZEKANA YESU AKAWA ANACHEZA MPIRA? YESU KASHIKA MPIRA,
MARA BEKi FULANI KAMKATA MTAMA AU TIMU YA YESU IMEPIGWA MAGOLI 6-0? kama
dhamiri inakataa kuwa YESU hawezi kufanya hvyo na sisi hatuwezi kufanya
hvyo.Tunatenda neno ambalo YESU anaweza kulitenda.
(iv)
Asili au sifa za Mashabiki wengi wa jambo hilo, vinara wa jambo hilo ,
JE NI MATAIFA? Kama wanaongoza ni mataifa, basi nyuma ya jambo hilo kuna
mashetani (UFUNUO 18:2-3,23) Mataifa yote yanapokuwa wanachukuliwa
hivyo katika jambo hilo, ndio vinara, mashabiki, kwa namna hiyo hiyo
uchawi unavyotajwa lazima tujue kuna roho za mashetani. Ukiona vinara au
viongozi ndio waasherati au walevi, wavuta bangi. Hawa wanaotajwa
washauri wa mambo ya kifundi katika timu hizo ndio wachawi wa timu.
(iv) Misingi ya mpira
Misingi
ya ushetani pekee ndiyo inayo ufanya ushabiki wa mpira uwe na nguvu na
kushangiliwa na mataifa.Ni rahisi sana kutoa ofa ya mpira kwa mshabiki
na ukashangliwa kuliko kusaidia masikini wanaoteseka na adha ya dunia
hii ukasifiwa huu mwezi mtukufu”.
Ni
heri mtu Yule atoae sadaka na kufuturisha wanyonge kuliko anaetumia
milioni za fedha kufadhili mpira kwa dk 90 tu .. Yamkini huenda ndiyo
maana juzi ile timu ilifungwa chanzo kikawa ni hiki (washabiki kumradhi)
Kwa wale wanaokumbuka kisa cha mfalme suleimani hapo utagundua ndipo mpira siyo kusudi la Mungu;
(a).
Ukisoma hiki kisa vizuri utagundua kile kisa cha mfalme suleiman na
taranta za dhahabu 666 na zilivyopokwa na mpinga kristo, ambapo makombe
ya dunia ya mpira yanaandaliwa kwa dhahabu.
(b).
Ukiendelea kusoma vizuri utaona kuwa mfalme Suleimani akawa kaulaani
upepo, na alisema pia pamoja na utajiri wote huu ni sawa na kujilisha
upepo, hilo neno upepo, lilikuwa na maana ya bure kabisa, na baada ya
hapo kilitengenezwa kitu mithili ya mpira kikajazwa upepo ili
kudhihirisha u-bure huo usiofaa machoni pa Mungu... HUO UPEPO ndio
unaojazwa mipira hadi leo na kukimbizwa kwa kulenga magoli.
(c).
Kile kitufe mithili ya mpira chenye upepo, kilichezwa kwa kulenga
katikati ya milingoti miwili mithili ya magoli na kushangiliwa na kerubi
akiwa ndiyo mwamuzi (REFA).
(d).
Wanafunzi wa yesu walikuwa 12, ukiondoa yule mmoja YUDA, walibaki 11
wenye Haki. Hao 11 ndio waliofungwa nira za kristo, lakini shetani hapo
Kageuza, kwa kuweka wachezaji 11 katika team ya mpira, jiulize kwanini
asingeweka 15? hao kumi na moja ndiyo wanaoshindana na kufungwa kwa
mchezo wa kulenga ktk ya milingoti (magoli).
(e). Katika mchezo shetani ndipo alipouteka ulimwengu kwa kugeuza ahadi za Mungu.
Ukisoma
bibilia Mungu kasema "Nitabariki kazi ya mkono yenu" lakini hapo
shetani akageuza, wacheza mpira ndiyo wanaolipwa pesa ndefu zaidi kwa
mda mfupi sana.. Maanake Hapo shetani aligeuza baraka za mikono kuwa za
miguu (Agano la mapinduzi); Kama vile kule bustani ya edeni nyoka
alivyogeuza.
(v) Clubs
kubwa duniani, na waanzilishi wa hizo clubs na waendeshaji wa hizo clubs
ni waabudu shetani(Devil worshipers) hata logo na majina ya clubs zao
ni za kishetani aghalabu;
(a) Manchester United (The Red Devils)
Ilianzishwa
1878 nchini England.Wanatumia rangi nyekundu na jina lake ni "Red
Devils" yaani mashetani wekundu.Logo yao kuu ni kiumbe wa kipepo mf
shetani/jini kashika uma wenye meno matatu na juu ya kichwa chake kavaa
crown ya kifalme,maana yeye ndiye mungu/mfalme wa Kuzimu & motoni
(b) Arsenal
Ilianzishwa
jijini London mwaka 1886.Mmoja wa waanzilishi wake ni pamoja na Peter
Healwood ambaye ambaye alikuwa ni wanachama wa freemasons.Wanatumia
alama ya silaha ya kivita (fataki) yenye magurudumu mawili kwaajiri ya
kuisafirisha kutoka station moja mpaka nyingine.Hujiita"The Gunners".Ni
kampuni ya waunda silaha za kivita/maangamizi.
(c) Chelsea (The blues)
"Chelsea"
ni kampuni ya pombe iliayonzishwa mwaka 1836 na ikazinduliwa rasmi
14/3/1905.Wanajiita "the blues" kwa kadiri ya waabudu shetani hiyo ni
blue satan kwa maana ktk lugha ya kiingereza hakuna wingi wa
"blue",hivyo ile "s" humwakilisha shetani wa bluu aishiye moto usio na
moshi(non luminous flame satan).Wana logo ya pepo/jini/shetani
lililoshika na funguo za kuzimu(mamlaka za giza)
(d) Real Madrid (The white)
Ilianzishwa Hispania tarehe 06/03/1902
Wanatumia
alama/Logo ya crown na inamaandishi " FMC" imetokana na kampuni ya
kamali Bwin (Beat & Win) ni kamali ni kinyume kabisa na mpango wa
MUNGU.
Kwa haya tu machache ktk suala la mpira na baadhi tu ya clubs,kuna utukufu wa MUNGU hapo?
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***
0 comments:
Post a Comment