Ikiwa ni hitaji kulitangaza jina la BWANA katika miji mbalimbali Duniani pamoja na JIJI la Dar Es Salaam,ikikadiliwa kwa sasa nusu asilimia(50%) ya wakazi wa dunia wanaishi mijini na kufikia 2050,sabini na tano asilimia(70%) ya wakazi wa dunia watakua wakiishi mijini...
Hivyo hitaji la kuwa na huduma ya kuwaandaa wakazi hawa kumpokea MWOKOZI wao,kumpokea MWOKOZI huyu kutafanyika huduma mbalimbali ikiwepo;-
- Kuwatembelea katika nyumba zao na maofisini kuwalika katika mikutano mbalimbali ya neno la Mungu
- Matendo ya huruma,kwa kugawa mahitaji kama nguo,pesa na chakula pale inapowezekana
- Kufanya usafi katika mazingira yalikithiri kwa usafu hili ni kuwasogeza karibu wapendwa hawa kuhisi upendo wa BWANA upo nao pia..
- Kutembelea wagonjwa na kuwapa dawa wahitaji wa huduma hiyo pia kutakuwa na uchangiaji damu kwa wahitaji husika..
Hapa Dar Es Salaam ikiwa na takribani vituo 123 vya mahubiri haya kwa miji mikubwa,kutakuwa na masomo ya;AFYA,KAYA NA FAMILIA, VIPINDI VYA UIMBAJI NA MAHUBIRI.
*** TUMA PICHA NA HABARI KWA WATSUP SASA NO 0717-367 693***




0 comments:
Post a Comment