Sunday, January 04, 2015

HABARI KWA HISANI YA MTWARA SDA CHURCH BLOG(http://www.mtwarasda.org)
Kanisa la Waadventista Wasabato Mtwara limefanya ibada ya pekee kufungua mwaka 2015. Katika ibada hiyo, mchungaji wa mtaa wa Mtwara Pr. Zetti Ndola amewaasa washiriki kujitoa katika kuifanya kazi ya Mungu mwaka huu. Mchungaji Ndola amesema hakuna haja ya kukataa kushiriki katika kazi ya Mungu pale tunapo hitajika kufanya hivyo.
Mchungaji Ndola amewakumbusha waumini kuwa Mungu anao watendakazi wengi hivyo usipo kubali kumtumikia mtu mwingine atachukua nafasi yako na hautapata mbaraka.
Mara baada ya hubiri la pekee Mchungaji Ndola alitoa wito kwa waumini kujiweka wakfu na kujirekebisha pale walipo anguka mwaka uliopita. Kwakweli Sabato ya leo ilikuwa ya pekee sana na Mungu amenena na wana na binti zake kupitia mtumishi wake Mchungaji Zetti Ndola.
Waumini wakiwa tayari kwa huduma ya kuwekwa wakfu.
Mchungaji Zetty Ndolla akitoa wito kwa waumini


****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0789 243 413 NA 0717 367 693***

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA