Tuesday, June 23, 2015

Mchungaji Mwakalindile mkurugenzi wa Redio ya Morning Star asubuhi ya leo akitoa mada juu ya mambo muhimu katika uletaji watu kwa Bwana kwa kutumia Redio  pale tunapoandaa vipindi. 
Mchungaji Mwakalindile mkurugenzi wa Redio ya Morning Star asubuhi ya leo akitoa mada juu ya mambo muhimu katika uletaji watu kwa Bwana kwa kutumia Redio  pale tunapoandaa vipindi. 
Pichani ni Mrs.Jullie Ochieng mkufunzi wa semina hizi toka nchini Kenya.
Mchungaji Mussa Mika ni moja ya wakarimani katika semina hizi..
Mchungaji Steven Bina ni Mkurugenzi wa mawasiliano toka Divisheni akifatilia mkutano mapema leo ndani ya kanisa la Waadventista Wasabato Arusha Mjini Kati.
Idara ya Mawasiliano ni kitu cha umuhimu sana katika maisha yetu hasa kwenye kipindi hiki,Mchungaji Mwakalindile ameeleza muhimu wa vifaa vya Mawasiliano na teknolojia inapozidi kuongezeka basi kuna kila haja ya kutumia kwa ukaribu sana vyombo vya mawasiliano mfano mama Ellen G White alitumia teknolojia hii kwa kuchapisha magazeti ya unabii kwenye karne ya 19 na akishauri kuwa siku za usoni njia za kipindi chake za Mawasiliano zisitumike kwenye kipindi cha sasa tokana na teknolojia.
Kanuni chache za ufanisi wakati wa uandaaji wa habari na kuwa mwanamawasiliano mzuri.1.Jenga mazoea ya kuongea vitu ambavyo unayafahamu vizuri na kutumia muda wako vizuri kujiandaa na kusoma hasa kwenye uwasilishaji wa habari.
2.Wafahamu wadhira au watu unaowafikishia ujumbe na kuwa ni waina gani hasa kwenye vyombo vya habari uku ukijua unasikilizwa na watu wa rika nan chi zote za Dunia tena wakiwa kwenye aina tofauti tofauti za kipato.
3.Toa ujumbe unaogusa mahitaji ya watu mfano kwa wana masoko na wafanya biashara kuona mahitaji na changamoto zao na kuongea vitu vinavyowagusa watu
4.Unapoogea na watu wafanye hadhira waone kama unaongea na mtu mmoja na tena kwa uchangamfu na angalizo likiwa mahubiri yetu yawe yanayolingana na mahala tulipo na kupunguza kelele kwani vifaa vya studio vinanguvu ya kunasa sauti.
Tv-unapoongea kwenye tv ni muhimu pia kuwa makini kwa muktaza wa muonekano wako kama kuweka kidole puani.
5.Zungumza kwa kutumia maneno mazuri wala sio yanayouumiza kwa lugha nzuri ambayo sio ya lazima ambayo yataleta picha nzuri kwa jamii ya vyombo vya habari ndio chachu ya kuleta ujumbe huu wa tumaini.
6.Ni vizuri yakaambatana na maandishi itasaidia kuongea kwa muda na mpangilio mzuri ukiwa ndani ya Redio na ikipendekezwa kuwa mtu anayesikiliza atoe mrejesho wa kile kinachohubiriwa.Na inaonekana pia mwanamawasiliano mzuri ni yule anayeweza kusikiliza
7.Muda ni kitu muhimu sana kwenye Mawasiliano na utunzaji wa muda
MULTMEDIA COMMUNICATION
Ni bora Zaidi kutumia njia nyingi za Mawasiliano kwa njia ya sauti na picha na hapa uwezo wa kujibizana kwa mtumaji na mpokeaji ili kupeana jumbe na kushirikiana.
****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA