Tuesday, August 16, 2016


WANKOTA KAPUNDA

Na Magreth Yohana,Shua Media
“Mateso ya mwenye haki ni mengi lakini Bwana humponya nayo.Zaburi 34:22

Kama wanadamu tuliumbwa na kuweka katika dunia hii lazima tupitie changamoto mbalimbli kiasi ambacho unaweza kukata tamaa na kuisi Mungu kakuacha na labda ukawaza Mungu hayupo  kutokana na kuwa labda huna hela,huna kazi,haujui hata maisha ya kesho yatakuwaje na huenda wakati huu umeshafukukuzwa sehemu uliyopanga kutokana na kodi ama una umwa ugomjwa ambao unakosa tumaini la maisha

  Wankota Kapunda ni binti mwenye umri wa miaka 24 ambaye amepooza miaka 4 iliyopita baada ya kupata ajali ya kugongwa na moja ya gari wa mwanafunzi  mwenzake ambayo walikuja nayo ndugu zake na kumsababishia   mifupa ya shingo kusagika na kuleta matatizo kwenye uti wa mgongo aliyosabisha tatizo hilo  siku ya mahafali yao ya kumaliza kidato cha sita shule ya sekondari wasichana  korogwe huko mkoani Tanga.

  Baada ya Wankota kupata tatizo hilo alikaa nyumbani kwa muda mrefu akiwa anangalia movie alitamani kuwa mwandishi wa muswada wa filamu na alifanikiwa jambo hilo la kuandika muswada kwa kupitia ulimi kutokana na upoozaji wa mwili mzima isipokuwa kichwa na hatimaye kufanikiwa kuingia katika mashindano ya kitaifa ya kuandika muswada kwa haraka na hatimaye kwa kupitia ulimi alifanikiwa  kuwa mshindi kwa  uandika  haraka  muswada wa huo yaliyofanyikia huko Zanzibari yakishirikisha nchi za nchi za Afrika Mashariki.

Baada ya hapo Wankota hukukata tamaa tena aliendelea kuwaza vitu vikubwa vitavyoweza kuisaidia jamii na watu wenye hali kama yake ambao wametengwa na familia zao kutokana na kuwa tatizo kama la kwake, ambalo linaitaji msaada mkubwa na  jamii inapaswa kuelimishwa jinsi ya kuwajali na kuwahudumia  vema  watu wenye tatizo kama la Wankota  kwa kupitia uigizaji wa movie ambao ataufanya alisema wankota.

Hayo nimewambieni mpate kuwa na Amani ndani yangu,Ulimwenguni mnayo dhiki lakini jipeni moyo na mimi nimeushinda ulimwengu.>>>Yohana 16:33.

Tumaini lipo jipe moyo ukijua Yesu amekushindia yote ya dunia yanapita na hayana budi kutokea alishinda ulimwengu hatakuacha usilie tena, usihuzunike kwa kuwa amesema yeye ameshinda ulimwengu, atakupa njia ya kukabiliana nayo yote endapo tu utaamua kumtumaini na kuomba katika kweli. Zaburi 24:1.


****TUMA PICHA NA VIDEO WhatsApp 0713 059 073 NA 0717 367 693***

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO "KIFO" TOKA KWA PADACK

MAHUBIRI YA USHINDI HATIMAYE 2017 HAYA HAPA